Bukobawadau

HUDUMA YA UPASUAJI WA WATOTO WENYE UGONJWA WA KICHWA KUJAA MAJI NA MGONGO WAZI YAZINDULIWA RASMI MKOANI KAGERA KATIKA HOSPITARI YA RUFAA YA MKOA

Shirika lisilokuwa la serikali la Friends of Children with Cancer Tanzania (FOCC TZ) lazindua rasmi huduma ya upasuaji wa watoto wenye ugonjwa  wa vichwa  kujaa maji na mgongo wazi mkoani Kagera katika Hospitali ya  Rufaa ya mkoa ambapo jumla ya watoto arobaini wenye tatizo hilo wanatajiwa kufanyiwa upasuaji  kuanzia Julai 25-26, 2015.
Mkurugenzi wa shirika la FOCCTZ Bw. Walter Miya katika uzinduzi huo alisema kuwa baada ya kutoa matangazo kupitia redio za jamii mkoani Kagera kwa muda wa siku mbili wameweza kupata watoto 70 wenye tatizo la vichwa kujaa maji na mgongio wazi kutoka katika wilaya zote saba  za mkao wa Kagera na nje ya mkoa.
Bw. Walter alisema watoto walioweza kufikishwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Kagera kwa msaada wa shirika lake ni 40 na watoto 30 wameshindwa kufika kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo wazazi kutokuwa na uwezo wa kuwasafirisha watoto hao, pia  changamoto ya wananchi kuwa na imani potofu ya kuwa watoto hao wamerogwa.
Huduma hiyo inatolewa  mkoani Kagera na shirika la Friends of Children with Cancer Tanzania wakishirikiana na Madaktari wataalam wa upasuaji huo kutoka Hospitali ya Rufaa ya Bugando pia kutoka katika kitengo cha Muhimbili Orthopaedic Instutite (MOI) kilichopo Hospitali ya Rufaa ya Taifa Muhimbili.
Daktari Gerald D. Mayaya kutoka idara ya upasuaji  Hospitali ya Rufaa Bugando akielezea chanzo cha tatizo la ugonjwa wa kichwa kujaa maji na mgongo wazi alisema kuwa ni mishipa ya kusafirisha maji kichwani kuziba na kichwa huanza kuvimba ambapo kuna watoto huzaliwa na ugonjwa huo pia wengine upatwa na ugonjwa huo wakiwa tayari wamezaliwa  na  watu wazima pia hupatwa na ugojwa huo.

Lengo la kutoa huduma hiyo katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Kagera ni kupunguza gharama kwa wazazi wenye watoto wenye tatizo hilo  badala ya kwenda Bugando na muhimbili  wapate huduma hiyo karibu na maeneo yao. Pia kutoa ujuzi kwa wataalam wa haspitali ya Rufaa ya mkoa wa Kagera ili wawe wanatoa huduma hiyo katika hospitali hiyo. Alisema Mkurugenzi wa shirika la FOCCTZ Bw. Walter.
Mkuu wa mkoa wa Kagera Mhe. John Mongella baada ya kuzindua huduma hiyo na kutembelea wodi ya watoto wenye tatizo la vichwa kujaa maji na mgongo wazi alisema amejifunza mambo mengi  maana mwanzo alijua kuwa ugonjwa huo  kwa watoto huzaliwa nao kumbe hata mara baada ya kuzaliwa au mtu mzima anaweza kupatwa na ugonjwa huo.
Mhe Mongella alitoa wito elimu kutolewa kwa wingi ili wananchi waweze kujua kuwa ugonjwa huo unatibika ili wazazi na walezi waweze kuwaleta watoto wenye tatizo hospitali ili wakatibiwe. Pia aliwashukuru Shirika la FOCCTZ kwa kuzindua huduma hiyo ambayo aliita huduma takatifu kwani inaokoa maisha ya watoto walio wengi.

Wito, Mhe. Mongella alitoa wito kwa wananchi wenye uwezo kuweza kushirikiana na shirika hilo ili kuchagia huduma hiyo kuokoa  maisha ya watoto. Pia alitoa wito kwa Wanahabari wa mkoa wa Kagera na Tanzania kwaujumla kuelimisha jamii juu ya tatizo hilo ili liweze kupunguzwa kwa kiasi kikubwa.
Naye Vaileth John Makula (32) mzazi wa Gib Philimoni kutoka Wilaya ya Karagwe alilishukuru Shirika la FOCCTZ kuleta huduma hiyo Kagera maana anasema kuwa mwanae Gib alizaliwa katika hali ya kawaida na baada ya miezi minne tatizo la kuvimba kichwa lilianza na alimpeleka mtoto wake katika hospitali
Next Post Previous Post
Bukobawadau