Bukobawadau

UZINDUZI WA KAMPANI CHADEMA/UKAWA JANGWANI YATAPIKA

Mgombea urais kwa tiketi ya Chadema kupitia Ukawa, Mh Edward Lowassa akiongea na wakazi wa jiji la Dar waliojitokeza katika uzinduzi wa Kampeni za Ukawa katika viwanja vya Jangwani mapema leo.Mh Lowassa amesema kipaumbele chake kimoja wapo ni Elimu huku akisisitiza kuwa kampeni zao zitakuwa ni za busara na hekima bila kutumia matusi.
Mke wa Mgombea Urais kupitia Chadema chini ya mwamvuli wa Ukawa, Mama Regina Lowassa akitoa salamu kwa wakazi wa Jiji la Dar Waliojitokeza katika uzinduzi wa kampeni za Ukawa katika viwanja vya Jangwani leo.
Mgombea mwenza wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh Duni Haji akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la Dar waliojitokeza kushuhudia uzinduzi wa Kampeni za Ukawa leo katika viwanja vya Jangwani
Mwenyekiti wa Chadema, Mh Freeman Mbowe akiwasalimu wakazi wa jiji la Dar Waliojitokeza katika uzimduzi wa Kampeni za Ukawa zilizofanyika Jangwani leo.
Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Mh Freeman Mbowe (wa kwanza kulia) akiwa na wagombea urais kwa Upande wa Zanzibar na Upande Wa Bara na mgombea mwenza bara wakionyesha Kitabu chao cha Ilani ya Uchaguzi mwaka 2015 katika uzinduzi wa kampeni za ukawa uliofanyika katika viwanja vya jangwani.
Halima Mdee akihutubia
 
 Wagombea Ubunge katika majimbo ya Dar Es Salaam wakitambulishwa mbele ya wakazi wa jiji la Dar waliojitokeza kwa wingi katika uzinduzi wa Kampeni za Ukawa leo zilizofanyika katika Uwanja wa Jangwani.
 Mgombea ubunge wa jimbo la Kisarawe kwa tiketi ya CUF Kingwendu akisikiliza hotuba ya mgombea urais kwa tiketi ya Chadema chini ya Mwamvuli ya Ukawa
 Mwenyekiti wa NCCR Mageuzi, Mh James Mbatia akihutubia maelfu ya wakazi wa jiji la Dar Waliojitokeza leo katika uzinduzi wa Kampeni za Ukawa jangwani jijini Dar
 Waziri Mkuu mstaafu wa awamu ya tatu, Mh Fredrick Sumaye akihutubia wakazi wa jiji la Dar waliofika katika viwanja vya Jangwani wakati wa uzinduzi wa kampeni za Ukawa
 Umati wa watu waliojitokeza katika uzinduzi wa kampeni za Ukawa katika viwanja vya jangwani leo
 Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema na Mgombea Mwenza wakiwaaga watanzania waliojitokeza katika viwanja vya jangwani katika uzinduzi wa kampeni za Ukawa
Moja ya kifaa cha Kisasa kabisa aina ya Drone ambacho kilikua kikitumika kupiga picha kutoka anagani ambacho kimekuwa kivutio kikubwa kabisa kwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam leo katika viwanja vya jangwani .Picha zote na Josephat Lukaza wa Lukaza Blog




''Viwanja vya kufanyia kampeni tunanyimwa, mazikoni kwenda napo tunakatazwa. Hatuna haki kabisa'' Haji Duni #Jangwani #Urais2015
 Lowassa: Hata wakiiba kura wataiba nyingi lakini bado zitabaki za kutufanya kushinda #UkawaJangwani #Urais2015
 Lowassa: Jambo la kwanza katika Ilani, kipaumbele cha kwanza elimu, cha pili elimu, cha tatu elimu ‪#‎UkawaJangwani‬ ‪#‎Uchaguzi2015‬
 "Madawa ya kulevya yanapopita pale Airport na hayakukamatwa yakakamatwa South Africa Lowassa alikuwapo?"- Sumaye ‪#‎Jangwani‬ ‪#‎Urais2015‬
 ''Wapo watu waliofungwa na minyororo ndani ya CCM, na hawajui hatma yao hadi sasa wanaburuzwa tu'' Mbowe ‪#‎Jangwani‬ ‪#‎Urais2015‬
Next Post Previous Post
Bukobawadau