Bukobawadau

KONGAMANO LA ELIMU YA JUU LAFUNGULIWA JIJINI ARUSHA

Afisa Masoko wa Kampuni ya Global Education Link (GEL) wa Tawi la Arusha, Regina Lema akitoa maelezo kwa mmoja ya wageni waliofika katika maonyesho yaliyoandaliwa na wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Tume ya Vyuo Vikuu nchini, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) pamoja na Kamati ya Wakuu wa vyuo Vikuu nchini (CVCPT) yanayofanyika jijini Arusha sambamba na kongamano la saba la elimu ya juu lililoanza leo Oktoba 1 -2, 2015.
Baadhi ya wakuu wa vyuo na viongozi mbalimbali wa Taasisi zinazohusika na masuala ya elimu wakipata maelezo toka banda la GEL.
Mwanafunzi wa Chuo cha St. Joseph akitoa maelezo jinsi mfumo wa Mita za kipekee za kutoa umeme kufuatana na matumizi ya mteja ambapo hata kama wateja wapo kumi kila mmoja anaweza tumia kutokana na mahitaji yake.
Chuo Kikuu cha Muhimbili cha jijini Dar es Salaam kimeshiriki katika maonyesho yaliyoandaliwa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Tume ya Vyuo Vikuu nchini, Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi (NACTE) pamoja na Kamati ya Wakuu wa vyuo Vikuu nchini (CVCPT) yanayofanyika jijini Arusha sambamba na kongamano la saba la elimu lililoanza leo Oktoba 1 -2, 2015.
Mmoja ya washiriki ambaye amebuni mtambo wa kuchuja maji akitoa maelezo machache.
Mmoja ya washiriki ambaye amebuni mtambo wa kuchuja maji, akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Profesa Awadh Mawenya, Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania aliyeambatana na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya akiwaonyesha ubora wa chujio linalotumika kutoa maji safi na salama.
Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine nao wapo...
Mwakilishi wa Chuo cha CBE cha jijini Dar es Salaam, akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Profesa Awadh Mawenya, Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania ambaye aliambatana na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya akiwaonyesha jinsi wanavyozingatia ubora wa vipimo kwa kuweka alama katika mizani.
Mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Agha Khan cha jijini Dar es Salaam, akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Profesa Awadh Mawenya, Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania. amyeambatana na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya na viongozi wengine.
Mwakilishi wa Chuo cha Mwalimu Nyerere Memorial, akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Profesa Awadh Mawenya, Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania ambaye aliambatana na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya.
Mwakilishi wa Chuo Kikuu cha Mandela cha jijini Arusha, akitoa maelezo kwa Mgeni rasmi Profesa Awadh Mawenya, Mwenyekiti wa Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania aliyeambatana na Katibu Mtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu nchini (TCU), Profesa Yunus Mgaya.
Maprofesa wakiwa katika kongamano la saba la elimu ya juu 2015 lililoanza leo Oktoba 1 -2, 2015 jijini Arusha.
Washiriki wakiwa katika kongamano la saba la elimu ya juu 2015 lililoanza leo Oktoba 1 -2, 2015 jijini Arusha.
Next Post Previous Post
Bukobawadau