Bukobawadau

LOWASSA AMNADI JULIUS KALANGA KUWA NDIEANAFAA KUSHIKA MIKOBA YAKE

 Umati wa Wananchi wa Mji wa Monduli ambako ni Nyumbani kwa Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, wakionekana kushangiliwa kwa furaha pindi Chopa yake ilipokuwa ikishuka katika Uwanja wa Polisi Monduli, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni zake,  Oktoba 5, 2015.PICHA ZOTE NA OTHMAN MICHUZI.
Wananchi wa Mji wa Monduli wakionyesha upendo wao kwa Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, pindi alipowasili katika Uwanja wa Polisi Monduli, kulikofanyika Mkutano wa Kampeni zake,  Oktoba 5, 2015.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akihutubia Mkutano wa Kampeni, uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi Monduli Mjini, Oktoba 5, 2015.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, akimnadi Mgombea Ubunge wa Jimbo la Monduli kwa tiketi ya CHADEMA, Julius Kalanga, wakati wa Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015.
Mke wa Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, Mama Regina Lowassa akiwasalimia Wananchi wa Mji wa Monduli, wakati wa Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015.
Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye akiwahutubia Wananchi wa Mji wa Monduli, wakati wa Mkutano wa Kampeni za Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa, uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015.

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Monduli kwa tiketi ya CHADEMA, Julius Kalanga, akizungumza machache juu namna atakavyoweza kuendeleza pale alipoaishia Mbunge wao wa awali.

Mh. Joshua Nassary wa Arumeru Mashariki akitema cheche zake.
Mgombea Urais wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kupitia mwamvuli wa UKAWA, Mh. Edward Lowassa na Waziri Mkuu wa Zamani, Mh. Fredrick Sumaye, wakionyesha lundo la kadi za wanachama wa CCM wa Wilaya ya Monduli, waliozirudisha ili kuungana na Watanzania wote kwenye harakati ya Mabadiliko, wakati wa Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015. Kulia ni Aliekuwa Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Monduli, Rubein Ole Kuney akiejiunga na Chadema.

Aliekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki, Mh. Joshua Nassary, akizikusanya kadi za Wanachama wa CCM zilizorudishwa na kujiunga na Chadema, wakati wa Mkutano wa Kampeni uliofanyika kwenye Uwanja wa Polisi, Monduli Mjini leo Oktoba 5, 2015.














BUKOBAWADAU MEDIA tunaendelea kujitahidi kuripoti kampeni za uchaguzi kama sehemu ya majukumu yetu ya kila siku kuhakikisha wananchi wanapata habari. Pia tunatoa wito kwa Wagombea wa vyama mbalimbali wajitahidi  kutushirikisha ikibidi na kuchangia gharama za uendeshaji ..!

BUKOBAWADAU MEDIA tunaendelea kujitahidi kuripoti kampeni za uchaguzi kama sehemu ya majukumu yetu ya kila siku kuhakikisha wananchi wanapata habari. Pia tunatoa wito kwa Wagombea wa vyama mbalimbali wajitahidi  kutushirikisha ikibidi na kuchangia gharama za uendeshaji ..!
Next Post Previous Post
Bukobawadau