Bukobawadau

FAHAMU JINSI #RECRUITME INAVYOWEZA KUKUPA UJUZI UTAKAOKUSAIDIA KUPATA KAZI UITAKAYO

Na Jamiimojablog
Ujuzi, katika soko la ajira ni mali ambayo inahitaji matengenezo na uboreshaji. Kama mali nyingine yoyote, matumizi yake bora, hukuzalishia zaidi. Sababu nyingi zimetolewa katika kipindi cha miaka mingi kwamba kuna utofauti wa wazi baina ya mtu mwenye elimu aliyeko kazini na mwenye elimu bila kazi. Utofauti huo ni jinsi ujuzi wa watu hao wawili unavyotumika.



Vijana wengi wa Tanzania wana ujuzi waliopata kutokana na mafunzo mbalimbali, lakini baadhi yao kushindwa kutumia ujuzi walionao. Sababu pekee inayosababisha hili ni; mahitaji ya ujuzi katika soko la ajira hayako sambamba na ujuzi utolewao. Matokeo yake ni vijana kujikuta kwenye sintofahamu iliyosababishwa na mgongano wa kiujuzi. Ushindani mkubwa katika soko la ajira duniani ni kuongezeka kwa matumizi ya TEHAMA ambayo imechukua nafasi kubwa ya ajira za watu, na kama ajira inahitajika basi mtu ni lazima uwe na ujuzi maalumu.



Mwalimu mjini Arusha mwenye ujuzi wa TEHAMA ana nafasi kubwa ya kupata ajira kuliko yule asiye na ujuzi huo. Karani jijini Dar es Salaam mwenye ujuzi wa teknolojia ya juu ana nafasi kubwa ya ajira kuliko yule asiye na ujuzi huo. Tour guide mkoani Morogoro mwenye ujuzi wa mitandao ya kijamii na ulimwengu wa kidijitali ana uwezekano mkubwa wa kugundua fursa mpya kuliko yule asiye na ujuzi huo. Mwana masoko wa Mbeya mwenye maarifa zaidi juu ya matumizi ya mitandao ana nafasi kubwa ya kuvutia watu zaidi ya yule anayeendelea kutegemea mbinu za kizamani. Orodha ni ndefu.



Umewahi kujiuliza kwa nini Ronaldo, Messi, Rooney, Usain Bolt, Venus, Serena na wanamichezo wengine wameendela kutamba katika tasnia ya michezo kwa muda mrefu? Siri imelala katika kuboresha ujuzi wao. Ili umuhimu wa mtu uonekane katika  soko la ajira, lazima uwe na ujuzi husika na uendelee kuuongeza mara kwa mara.


Ujuzi unaweza kupatikana kupitia njia mbalimbali. Mtu anaweza kwenda shule; wengine wanaweza kufanya kazi na wazoefu. Mwingine anaweza pia kutumia muda kwenye mitandao na kupata ujuzi autakao. Miongoni mwa majukwaa ya kuaminika kwenye mtandao yanayokuja kwa kasi katika kutoa ujuzi na mafunzo bora na bure ni RecruitMe. Kupitia RecruitMe, unaweza kuokoa muda na fedha na bado ukapata kitu kilicho bora. Unaweza kuchagua mafunzo na ujuzi unaoutaka na kujifunza kwa muda mfupi sana. RecruitMe husaidia kuimarisha ujuzi wako, na kukufanya uwe yule mtu ambaye kila mwajiri angetaka kuwa naye. Anza sasa kuboresha ujuzi wako kupitia RecruitMe, ili upate kazi uitakayo bila wasiwasi. Kujiunga, tembelea: http://recruitme.co.tz/
Next Post Previous Post
Bukobawadau