Mwezi mmoja baada ya
kumaliza elimu yangu ya kidato cha sita 2009 February 12 huko jijini
Mwanza nilirejea nyumbani kwetu Mbeya.......
Nyumbani kwetu nipakawaida sanaa lakini nashukuru Mungu tulikuwa tunauwezo wa kupata chakula (asubuhi, mchana na jioni)
Nakumbuka siku moja niliwahi kusikia baba yangu akizungumzia kuhusu
swala la kuwasaidia yatima.. Wajane pia kuwatembelea wafungwa.......
Nilibahatika kupata kakazi ka kufundisha shule moja pale mtaani kwetu
jambo ambalo liliniwezesha kupata hela kidogo ya kujikim..... Baada ya
kulipwa niliwanunulia wazazi wangu zawadi japokuwa ilikuwa ndogo *****
siku hiyo jioni wakati wa Sala mama yangu aliniita faragha na
kuniuliza '' mwanangu Mau hivi toka uzaliwe ushaawahi kwenda
kuwatembelea watoto yatima? '' nilimjibu mama kwamba sijawahi......
Mama akaniambia basi siku moja jipange twende tukawatembelee '' lakini
mama kwa kitu gani hasaa tulichonacho ili tuwatembelee '' nilimjibu mama
yangu......... Mama alizidi kunielewesha kwamba chochote ukitoa kwa
Moyo basi hicho ni kikubwa sanaaa kwa Mungu......... Tulizidi kuongea
sana hatimae tulifikia muafaka kwamba jumapili tungeondoka......
Jumapili majira ya saa saba tulianza safari yetu mimi, baba na mama....
Tulifika salama na tulipokewa vizur sanaa na mda wa kukutana na watoto pamoja na kuwapa chochote kitu ulifika...............
Ilikuwa ni ngumu sanaa kwangu pale ambapo mtoto mmoja alikuja moja kwa moja kwangu....
Mtoto huyu alikuwa kati ya miaka 6 mpaka 7 (Maurine) alipokuja
alinirukia '' baba shikamoo.. Kwanini umeniacha hapa??? Leo si
tutaondoka wote?? '' Maurine alizidi kuongea huku analia na mimi
nililia pia kwa sababu ni wazi kwamba Sina mtoto lakini nilijua fika
mtoto yule anamis mapenzi ya wazazi wake na wengine wapo pale hawajui
kwamba wazazi wao hawapo tena duniani..........
Kiukweli nililia
sanaa baada ya kuona machozi ya binti huyu lakini nililia zaidi kwa
kuwa mimi sio baba yake japo sikuweza kamwambia ukweli....... Tulizidi
kupiga story na maswali yake mda wote yalikuwa magumu kwangu '' baba leo
si tutaondoka wote?? Naomba usiniache!!! Nilimwambia nakupenda na
sikuachi ***** niliendelea na kuwasalimia watoto wengine lakini Maurine
tulipokuwa tunapita aliwaambia watoto wote kuwa mimi ni baba yake na
aliwasisitizia kuwa tunaondoka wote!! Upande wa pili nilimuona baba
yangu na mama wakiwa wanafurahi pamoja na watoto wengine.... Walipiga
picha kadhaa na mimi pia nilijumuika nao..........
Mda ulisonga
mbele hatimae muda wa kuondoka uliwadia na watoto waliambiwa warudi
ndani kwenda kuoga....... Ulikuwa ni muda mgumu zaidi kwangu Maurine
alilia sanaa kitendo cha mimi kuonyesha ishara za kumuacha ðŸ˜ðŸ˜
nilimpa tsh 10000 nikamwambia '' nakupenda sana mwanangu basi nenda
ukaoge uje twende '' na niliahidi nafsi yangu kwamba ningekuja tena siku
nyingine......... Nlimuachia namba yangu ya simu lakini pia anuani
yangu.......... Aliondoka akiwa anaamini kwamba atanikuta pale pale ðŸ˜ðŸ˜......
Mara baada ya kuondoka Maurine safari yetu ilianza lakini roho yangu
ilifadhaika sanaaa mda wote hususani nikiyakumbuka Yale
maneno............... Mwezi mmoja badae baada ya kupata kale kamshahara
kangu nilifunga tena safari kwenda kumuona Maurine........
Nilifika kule na nlipokelewa vizuri sanaaa... Muda kidogo baadae
nililetewa barua ya Maurine ambayo ilikutwa kwenye begi Lake.....
Sister walinipa taarifa kwamba Maurine alipotea siku moja baadae akiwa
ananitafuta mimi. ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜.............
Walitoa taarifa polisi lakini mafanikio yalikuwa F..... Hatimae siku
nne baadae kadri ya maelezo ya sister mwili wa Maurine ulipatikana ukiwa
umeharibika sanaaa (amekufa) nililia sanaaaa
Nilikubaliana na
Ile hali ndipo nikaamau kusoma Ile barua ya Maurine '' NAKUPENDA SANA
BABA.... KWA NINI UMENIACHA?................
........!''Barua Ile ilikuwa ndefu japo hati yake ilikuwa bado ya kitoto
ila niliielewa sana,,,,,,,,,,, sikuamini kwamba niliyoyasikia ni kweli
ama ndoto............. ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜ðŸ˜
won't forget you Maurine...... Huenda ndicho kifo chako ulichopangiwa
ila naumia kwamba umekufa ukiwa unaamini mimi ni baba yako ðŸ˜ðŸ˜..............
Story hii ni ya kweli ila tu nimebadilisha baadhi ya majina kwa makusudi maalum...........
Nimesukumwa kuandika haya baada ya kuona kwamba wengi tupo tayari
kuchangia anasa kama vile graduation lakini mambo ya kusaidia wahitaji
kama
Wajane
Yatima
Wafungwa
Wagonjwa nk.
Tumeachana nayo ila kuchangia vitu vingine tupo tayari ili yule na yule
wakuone na upewe sifa (papaa fulani)........wewe unachangia nini
zaidi..tafakari chukua hatua.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comment:
Post a Comment