Kidoa aibuka kidedea Ijumaa Sexiest Girl 2015
Video Queen anayefanya pia filamu, Asha Salum ‘Kidoa’ akiwa na tuzo yake ya Ijumaa Sexiest Girl 2015 baada ya kuwafunika Elizabeth Michael ‘Lulu’ na Vanessa Mdee ‘Vee ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo Mbagala- Zakhem jijini Dar.
Kidoa (katikati) akiwasalimia mashabiki baada ya kutangazwa mshindi wa Ijumaa Sexiest Girl 2015.
...Akilia kwa furaha.
Kidoa akikabidhiwa tuzo na Mkurugenzi wa Hamadombe Distributor, Fatuma Makame.
...Akibusu tuzo.
Akiwa katika picha ya pamoja na mratibu wa shindano hilo lililodhaminiwa na kampuni ya uandaaji na usambazaji wa filamu ya Hamadombe Distributor, Amran Kaima (kulia).
...Akiwa na tuzo na cheti baada ya kukabidhiwa.
Mshindi wa Ijumaa Sexiest Girl 2015, Kidoa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Gazeti hilo.
(PICHA NA RICHARD BUKOS NA MUSA MATEJA/GPL)