Bukobawadau

RC DAR ES SALAAM APOKEA MSAADA WA MADAWATI 500 KUTOKA TIGO KWA AJILI YA SHULE ZA MSINGI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kushoto), akisalimiana na Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez mara baada ya kuwasili Shule ya Msingi ya Kawawa iliyopo Manispaa ya Kinondoni kupokea msaada wa madawati 500 kutoka Kampuni ya Simu ya Tigo Dar es Salaam leo asubuhi.
RC Makonda akisalimiana na wafanyakazi wa Tigo.
Ofisa Elimu wa Wilaya ya Kinondoni, Kiduma Mageni akizungumza katika hafla hiyo ya kupokea madawati hayo.
Ofisa Elimu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Raymond Mapunda akizungumza kwenye hafla hiyo kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kupokea msaada huo.
Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez  akizungumza katika mkutano huo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (katikati), akizungumza katika hafla hiyo wakati akipokea msaada huo.
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Kawawa wakipiga makofi wakati wa kupokea msaada huo.
Wanahabari nao walikuwepo kuchukua taarifa hiyo.
Viongozi na wafanyakazi wa Tigo wakifuatilia kwa karibu hafla hiyo.
Hapa ni furaha tupu kwa wanafunzi wa shule hiyo.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Simu ya Tigo, Diego Gutierrez na Mkurugenzi wa Kanda ya Pwani wa Tigo, Gooluck Charles wakiwa wamekaa pamoja na wanafunzi wa Shule ya Msingi ya Kawawa baada ya kampuni hiyo kuisaidia shule hiyo madawati 50 Dar es Salaamleo asubuhi. Tigo imetoa madawati kwa shule 10 za Manispaa ya Kinondoni ili kuunga mkono jitihada za Makonda za kuhakikisha wanafunzi wanakuwa katika mazingira bora ya kupata elimu.
Mwanafunzi wa darasa la saba wa shule hiyo, Joseph Proches akitoa neno la shukurani kwa Tigo kwa kuwapatia msaada huo wa madawati.
Walimu wakiwa kwenye hafla hiyo.
Wanafunzi wakiwa wamekaa kwenye madawati hayo.
Wanafunzi wakiwa wamekaa kwenye madawati hayo.


Na Dotto Mwaibale

KAMPUNI ya Simu ya Tigo Tanzania imetoa msaada wa madawati 500 yenye thamani ya sh.milioni 82.5 kwenye shule 10 za msingi katika mkoa wa Dar es Salaam ikiwa ni mchango wa kampuni hiyo katika kusaidia serikali kukabiliana na upungufu wa madawati katika shule za msingi nchini.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo Mkurugenzi Mkuu wa Tigo, Diego Gutierrez alisema mchango huo ni sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya kampuni hiyo ya kuunga mkono jitihada mbalimbali za kuleta maendeleo nchini.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda ameishukuru kampuni hiyo kwa msaada huo na kusema utawasaidia wanafunzi kupata elimu bora wakiwa katika mazingira mazuri hivyo aliwataka wanafunzi hao kuongeza bidii ya masomo yao. 
Next Post Previous Post
Bukobawadau