Bukobawadau

B/NEWZ:OFISA AJINYONGA KAGERA

Katibu wa Tume ya Utumishi na Nidhamu ya Walimu (TSD ) Wilaya ya Muleba, Manase Mkumbo amekutwa amefariki dunia kwa kujinyonga shambani mwake katika Kijiji cha Kyamyorwa wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Muleba Francis Isack amesema Mkumbo alijinyonga usiku kuamkia leo.
Amesema kabla ya tukio hilo alituma ujumbe wa maandishi kwa simu akimjulisha mwanae aliye masomoni kuwa amekata tamaa na maisha.
Isack amesema Mkumbo aliondoka Muleba kwenda kukagua mashamba yake kijijini ambako aliandika ujumbe huo na kununua kamba ya katani na kujinyonga.
Next Post Previous Post
Bukobawadau