Bukobawadau

TUSIFANANE NA WALE WAPENDAO KUONEKANA SAA MBILI KAMILI USIKU

Habari zenu wana Bukoba na Kagera kwa ujumla.
Mkoa wetu kwa miakaa michache ya hivi karibuni mpaka sasa umekuwa katika orodha ya mikoa iliyo katika kiwango cha juu cha umasikini. Na kila mara watu wengi tumekuwa tukisema mengi mitandaoni na matamasha mbali mbali juu ya kuuinua mkoa wetu kutoka tulipo ili kupiga hatua ya maendeleo.
Ingawaje hatua ya maendeleo si OVERNIGHT DREAM tayari maendeleo la hasha. Lakini kwa matamasha harambee na maandishi ya mitandaoni hazina kasi tena ni kama zinafanywa kama zima moto bila malengo halisi ya uendelevu.
 Mara nyingi malalamiko yetu yamekuwa na pressure wakati wa mjadala, siku ya kwanza facebook au whatsap au kwenye harambee, tamasha, kongamano tukitoka hapo yanaisha nguvu na hakuna wa kujadili tena.
Na mara nying ikikaribia Desemba kila mwaka ndiyo unasikia tunajinadi tukutane Bukoba mwisho wa mwaka huu tutakuwa na mkutano wa kujadili fursa na maendeleo ya mkoa wetu na maneno mazuri ya Kagera imeshuka jamani omuka nshoni mara kamunobele, mara standi mara mji ulivyochoka watu wake tulivyochoka , elimu na uchumi viko chini si kama zamani haya yanasikika sana wakati huo na tukifika kwenye kongamano tunajadili vizuri na kuondoka na way forward lkn je baada ya January kuna kinachoendelea?
 Kama hakuna Je, tukifananishwa na wale watu wapendao kuonekana saa mbili na kamili usiku ni uongo? Nini maana ya saa mbili usiku. Hapa nimemaanisha saa mbili usiku ndiyo mida ya taarifa za habari kwa vituo vingi ya radio na television so watu wengi hufanya mambo na kualika vyombo vya habari ili waje waonekane kweye habari saa mbili usiku muda ambao watu wengi wanaangalia au kusikiliza. Uonekane hasa wale watoao misaada kwa jamii na makundi mbali mbali au kwa namna yoyote nyingne.
Je kwa maandishi na malalamiko na makongamano tuliyofanya tuna sustainability plan? Je tuliyojadili kila mara kwenye makundi ya online jumuisho lake ni nini? JE NI NANI WA KULAUMIWA KAMA SI MIMI NA WEWE?
Ingawa kuna msemo unasema wazawa pekee hawawezi kuleta maendeleo kwao mpk iwepo interaction ya watu kutoka nje lkn sijui km usemi huu unajitoshereza na kukamilisha udhaifu wetu eti tusubiri muingiliano ndo tupige hatua.
 Je viongozi wetu wenye kutuongoza wameguswa vipi na hali ya mkoa? Kama WABUNGE, WATAWALA, MADIWANI VIONGOZI WENGNE WOOTE NA JAMII KWA UJUMLA tukiguswa kwa hakika tukaondokana na habari za zima moto za kujadili maendeleo kwa vipande na tukaacha mpk decemba nyingne na tukaishia mikoani huko maana kwa sasa si ajabau ukakutana na mtu mkoani akasema mimi kwetu Zanzibar au Arusha au Mwanza mtu anajisifia ATI INYE OGU MWAKA GWA KASHATU…. TINKAGYAGA BUKOBA NINGAYO KUKOLAKI? Haya buzima tubandize omumaka gaitu nu tugainunule
Kama hatutabadilika na kulichukulia umakini suala hili la uendelevu tukajadili bora liende na kurudi Dar kimya basi tujiandae kuagiza kahawa Kilimanjaro, Mbinga, Mbeya, Kasulu pamoja na ndizi Kilimanjaro na Uganda
Mwesiga Johnstone Samwel
Next Post Previous Post
Bukobawadau