Bukobawadau

Mahakama ya rufani ya Tanzania yamhukumu Kunyongwa Mkuu wa Upelelezi Kinondoni

Mahakama ya rufani ya Tanzania yamhukumu kunyongwa hadi kufa aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi Kinondoni, Christopher Bageni katika kesi ya vifo wafanyabiashara wa madini.
Katika kesi ya msingi Bageni na wenzake,walidaiwa kuwaua kwa kukusudia wafanyabiashara Sabinus Chigumbi,Ephraim Chigumbi, Martias Lunkombe na Juma Ndugu aliyekuwa dereva wa teksi wa Manzese.
Pia ilidaiwa kwamba, watuhumiwa hao walitenda makosa hayo January 24 2006,katika msitu wa Pande,uliopo wilaya ya Kinondoni,baada ya kuwakamata wafanyabiashara hao sinza baada ya kuja jijini Dar Es Salaam kufanya biashara.
Next Post Previous Post
Bukobawadau