Bukobawadau

SBL yaanza kuuza bia Kenya

Dar es Salaam, Februari 20, 2017- Kwa mara ya kwanza, Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) imeanza kuuza nje ya nchi  bidhaa zake katika  soko la kikanda,  eneo la kwanza  likiwa ni nchi jirani ya Tanzania kwa upande wa Kaskazini, Kenya.
Shehena ya kwanza ya bia  inayofahamika kama Allsopps ilisafirishwa kwenda Kenya wiki iliyopita na hivyo kukiweka kiwanda cha SBL kuwa mmoja wachangiaji wakubwa katika soko la kanda.
 Akizungumzia kuhusu hatua hiyo, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa SBL, John Wanyancha alisema; “Hii ni hatua nyingine ya kufurahisha  katika kampuni yetu  na kimsingi kwa  bidhaa zetu. Ukweli unabakia kwamba kumudu  kupenyeza ndani ya soko la Kenya  kunaonesha kuwa  ubora wa bidhaa zetu  sio tu kwamba unakubalika  na wateja wetu wa ndani bali pia  zinakubalika katika soko  kubwa  la kikanda.”
Wanyancha alisema kuwa SBL inaangalia  uwezekano wa kupanua mauzo ya biashara katika masoko mengine ya kikanda, hatua ambayo iko  katika mkondo wa kuhamasisha  Jumuia ya Afrika Mashariki  na kada nyingine za kiuchumi  kuongeza biashara yake  ya kuvuka mpaka  ndani ya ukanda huo.
 SBL imekuwa inazalisha aina za bidhaa  zinazotambulika kimataifa  kama vile Pilsner Lager,Tusker Lager, TuskerLite, Kibo Gold, Guinness Stout, Uhuru, The Kick pamoja na bidhaa kuu ya Serengeti Premium Lager-ambayo peke yake  imeshajizolea medali  kumi zinazotambuliwa kimataifa.

Next Post Previous Post
Bukobawadau