Kuwa kiongozi mzuri kwa mtu yeyote ni lazima uwe na huruma,
kuwajali watu waliokaribu na wewe na wasiokuwa karibu, kusikiliza kero
za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi, lakini jambo muhimu sana kutimiza
ahadi unazozitoa mbele ya wale unaowaongoza na mwisho kuguswa na
matatizo ya wenzako na kuwatia faraja.
Kwa hayo yaliyotajwa hapo juu ameyatimiza Mkuu wa Mkoa wa Kagera Meja
Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu kwa mama mjane Shemsha Rajab kutoka
Kata ya Kashai Mtaa wa Rwome Manispaa ya Bukoba ambaye ni mlemavu wa
mguu (ana mguu mmoja na mguu wa pili umekatikia gotini) na anatumia mguu
bandia.
Mkuu wa Mkoa Mhe.
Kijuu kwa fedha zake takribani shilingi 700,000/= (laki saba)
amemnunulia mguu bandia na kumkabidhi leo tarehe 11/05/2017 ofisini
kwake. Akiongea kabla ya kumkabidhi mama huyo mguu bandia Mkuu wa Mkoa
alisema kuwa alikuwa anatimiza ahadi yake aliyoitoa mwaka jana Juni 27,
2017 kwa mama Shemsha alipotembelea Haospitali Teule ya Wilaya ya
Missenyi Mugana.
“Nilipotembelea Hospitali hiyo kwenda kukagua shughuli za upasuaji
wa akina mama wenye tezi shingo ambao ulikuwa umefadhiliwa na Hospitali
Teule ya Mugana kwa kushirikaiana na Mzee Raza Fazar wa mjini Bukoba
kupitia katika mradi wake wa matibabu (Izaas Medical Project) niliguswa
na mama huyu kwani niliona jinsi anavyopata shida na nilimuhaidi
kumpatia mguu bandia mpya.” Alieleza Mhe. Kijuu.
Mama mjane
Shemsha Rajabu alimshukuru Mkuu huyo wa Mkoa na kusema kuwa anaguswa na
matatizo ya wananchi wake. Pia alimshukuru sana Mzee Raza Fazar kwa
huruma yake ya kuhakikisha anawahudumia wananchi wenye matatizo hasa
wale wasiokuwa na uwezo kwa kuwapatia huduma za matibabu bure kupitia
mradi wa matibabu wa Izaas.
Kutoa ni moyo usambe ni utajiri kama wahenga wa zamani walivyosema, kila
mmoja wetu anatakiwa kumsaidia mwenzake mwenye matatizo ili wenye
matatizo wajisikie kama binadamu wenzao. Mama Shemsha alisema kuwa mguu
wake wa bandia wa kwanza aliupata mwaka 1997 lakini kwa sasa mguu huo
ulikuwa hautumiki tena kwasababu unyayo wake ulikuwa umeharibika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comment:
Post a Comment