Bukobawadau

WASANIFU MIRADI YA UJENZI WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI


Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, akizungumza na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Eng. Jackson Masaka pamoja na viongozi wengine wa wilaya hiyo, wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, akitoa maelekezo kwa Mkandarasi China Henan International Corporation anayejenga daraja la Sibiti lenye urefu wa mita 82 na barabara za maingilio kwa kiwango cha changarawe zenye urefu wa KM 25, alipokagua ujenzi wa miradi hiyo mkoani Singida.

Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Singida Eng. Leonard Kapongo, akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa (wa pili kulia), alipokagua ujenzi wa daraja la Sibiti lenye urefu wa mita 82 na barabara za maingilio kwa kiwango cha changarawe zenye urefu wa KM 25, mkoani Singida

Mhandisi Mshauri Mr. Sunil Singh, akimuonesha Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, uwekaji zege katika moja ya boksi kalvati kubwa linalojengwa katika barabara za maingilio ya daraja la Sibiti, mkoani Singida.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa (katikati), akioneshwa na Mhandisi Mshauri Mr. Sunil Singh (kulia), nguzo zilizojengwa kushikilia daraja la sibiti, alipokagua ujenzi wake jana, mkoani Singida. Kushoto ni Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS), mkoa wa Singida Eng. Leonard Kapongo.

Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Sekta ya Ujenzi) Mhe. Elias Kwandikwa, akizungumza na wananchi wa kata ya Mpambala wilayani Mkalama, wakati alipokagua ujenzi wa daraja la Sibiti lenye urefu wa mita 82 na barabara za maingilio kwa kiwango cha changarawe zenye urefu wa KM 25, mkoani Singida.

Muonekano wa nguzo tatu zitakazoshikilia Daraja la Mto Sibiti lenye urefu wa Mita 82 na upana wa mita 10.5. Daraja hilo ni kiungo muhimu kwani litaunganisha Wilaya ya Iramba na Mkalama mkoani Singida na Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu.
Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano
Next Post Previous Post
Bukobawadau