Bukobawadau

NYOTA WA EMPIRE AZURU NYUMBANI BUKOBA

Msanii @kokugonza mwenye asili ya Kagera,mtoto wa mzee Longino Mugalura wa Kiziba Kashasha anaye ishi na kufanya shughuli zake nchini Marekani ameonekana katika baadhi ya maeneo ya Bukoba akifanya shughuli za kijamii mbalimbali ikiwemo kutembelea shule ya Josiah Girls na kuzungumza na wasichana wa shule hiyo pamoja na kutembelea Kijijini kwao Kiziba -Kashasha.Msaanii huyu amewahi kushiriki katika tamthilia ya EMPIRE inayoshirikisha wasanii wakubwa akiwemo Terrence Howard,Taraji P Hensen wengine ni Neyo na 50 Cent.
Ikumbukwe mnamo April 2016 mtandao wa Bukobawadau ulizungumzia nyota huyo mwenye asili wa Bukoba na wakajitokeza ndugu na jamaa wakadhibitisha hilo.
Nyota wengine walioshiriki tamthilia ya EMPIRE ni pamoja na Naomi Campbell ,Estelle ,Alicia Keys na wengine kibao.
Next Post Previous Post
Bukobawadau