Bukobawadau

MULEBA YASHAURIWA KUSOGEZA HUDUMA ZA AFYA KWA WANANCHI

HALMASHAURI ya Wilaya ya Muleba mkoani Kagera imeshauriwa kusogeza huduma za afya  kwa wananchi  kwa kutekeleza mpango wa serikali  wa kujenga  zahanati kila kijiji sambamba na kuwa na mpango mkakati  wa kudhibiti  mlipuko wa malaria pindi unapotokea.
Ushauri huo ulitolewa na mkuu wa wilaya hiyo Lembris Kipuyo baada ya kutokea kwa mlipuko wa malaria wilayani humo  kipindi cha mwezi Mei na Juni mwaka huu na kusababisha vifo vya watoto wengi chini ya miaka mitano.
Kipuyo alisema kwa sasa katika wilaya hiyo maambukizi ya malaria ni asilimia 22 ambapo alidai kuwa kiwango hicho bado ni kikubwa na kuwataka watendaji na viongozi wote wa halmashauri hiyo kuhamasisha wananchi umuhimu wa kutumia vyandarua na kusafisha mazingira ili kuharibu mazalia ya mbu.
Alisema ni wajibu wa  halmashauri kuwasiliana na idara ya afya  ili iwapatie wataalam wa  afya wa kutosha yakiwemo madawa na vifaa tiba vya kutosha ili kukabiliana na tatizo la malaria katika wilaya hiyo.
Na Ashura Jumapili.
Next Post Previous Post
Bukobawadau