Bukobawadau

Mkurugenzi wa Kimoda Tanzania atoa mafunzo Wilayani Misenye

Shirika lisilo la kiserikali la kimoda Tanzania lenye makao yake makuu Dar es salaam limeweka mikakati ya kubaini vyanzo vya ongezeko la watoto watoto wa mitaani mkoani Kagera.

Hayo yameelezwa na mwenyekiti wa shirika ilo Bi Dorotia Emanuel katika afla fupi ya kutoa misaada ya nguo na vyakula kwa watoto wa kijiji cha Ishozi wilayani Misenye.


Naye mjumbe wa Tacaids taifa Bi Reocadia Rugambwa amesema kuwa Tacaids kwa kushirikiana na Kimoda wametoa mafunzo maalumu ya watoto wanao ishi katika mzingira hatarishi ili kuweza kupata viongozi wa badae.

Pichani ni mjumbe wa wa Tacids taifa Bi Reocadia Rugambwa .

Bi Dorotia amesema nchi imekuwa ikipoteza wataalam wengi kutokana na kutowajali watoto wadogo.Pia amesema Kimoda Tanzania kwa kushirikiana na halmashauri ya Misenye itaendesha zoezi la kufanya utambulizi wa watoto wanaoishi katika mazingira magumu Wilayani humo.
Mr Mwemezi Kabigumila mwakilishi wa Radio 5 Mkoani kagera akiwa amembeba Mtoto mwenye ulemavu Neema Desney mwenye miaka 12.

Ndg wadau kutoa ni moyo jamani kama unao uwezo wa kutoa chochote kile ulichonacho unaweza kumsaidia mtoto huyu ambae awezi kutembea wala kuongea na awezi kufanya chochote kile.
Misaada mbalimbali ilimetolewa ikiwa ni pamoja na chakula na mavazi

Kikundi hicho pia kinamradi wa mbuzi wa maziwa.kama unaweza kujiomea katika picha

Next Post Previous Post
Bukobawadau