Bukobawadau

WAKRISTO WAANZA FUNGA YA JUMATANO YA MAJIVU;matukio ya kanisa Katoliki.

Kama inavyo eleweka kufunga ni tendo la kibinadamu na ni tendo linalo gusa maisha ya kiroho na leo hii Wakristo wameanza kipindi cha kwaresima  yaani siku arobaini za mfungo.
Mdau  pichani ni Bi Happy mara tu baada ya kupakwa majivu  kwenye paji la uso.
Ndg  Peter Matagi katika mwanzo wa kujinyenyekesha kwa mwenyezi Mungu .
Kushoto ni Fr.Denis Rweyunga akiubiri juu ya funga.
Bi Happy Kushoto na Mr Temmy AlphonceAdd caption
Kanisa kuu la Bikira Maria Mama wa huruma la katoliki  Jimbo la Bukoba(ujenzi ukiendelea)

Fr.Faustine Kamuhabwa(Baba paroko) akibariki majivu katika ibada ya kupaka majivu hii leo.
Waumini waliohudhuria ibada ya kupaka  Majivu
 Mfungo uliagizwa toka Paradizini. Mungu alimtaka kumtiisha binadamu ili awe chini yake na kujisikia kuwa ni kiumbe. Kumbe katika kuwa na urafiki mwema na Mungu kwatakiwa kujikatalia, ndiyo maana Mungu anamwagiza Adamu kufunga na kujikatalia. Kwa hiyo kila mfungo humkumbusha mfungaji urafiki wake asili na Mungu na jinsi ulivyopotea.

BUKOBAWADAU BLOG TUNAWATAKIA WAKRISTO WOTE KWARESIMA NJEMA NA YENYE HERI!!!




Next Post Previous Post
Bukobawadau