Bukobawadau

IJUWE HALMASHAURI YA WILAYA YA BUKOBA VIJIJINI ;Halmashauri yenye historia kabla ya Uhuru wa Nchi yetu!!

 Mwonekano wa jengo la Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Vijijini(Chember)lililopo  Mjini Bukoba.

Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ni moja kati ya Halmashauri za Wilaya nane zilizomo katika Mkoa wa Kagera. Halmashauri ya Wilaya hii ni miongoni mwa Halmashauri kongwe nchini kwani imekuwepo tangu kabla ya Uhuru wa Nchi yetu. .
 Jengo hili limejengwa kabla ya Uhuru  na jiwe la msingi limewekwa  4/11/1958 na Senior Proviancial Commissioner Ndg S.A. Walden.
Kijiografia Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba ina jumla ya eneo lipatalo hekta 284,100, kati ya hizo hekta 2,293 ni eneo linalofaa kwa kilimo hekta 660 ni eneo la malisho ya mifugo, hekta 300 zimefunikwa na maji.

 Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba upande wa mashariki inapakana na Ziwa Victoria na Halmashauri ya Manispaa Bukoba, kaskazini inapakana na Wilaya ya Missenyi, magharibi inapakana na Wilaya Karagwe na kusini inapakana na Wilaya ya Muleba.

 Wilaya ipo katika vipimo vifuatavyo; Nyuzi 3 o 0045-31 o 00' Mashariki mwa Greenwich na nyuzi 1 o 00-3 o 00' kusini mwa Ikweta. Ipo milimita 1200 juu ya usawa wa Bahari. Hali hii inafanya Halmashauri ya Wilaya Bukoba kuwa na misimu miwili ya mvua yaani Vuli ambayo huanza mwezi Septemba na kumalizika mwezi Desemba na masika ambayo huanza mwezi Machi na kumalizika mwezi Juni. Kipindi cha Julai hadi mwanzoni mwa mwezi Septemba ni kiangazi na kipupwe uanza mwezi Januari hadi mwezi Februari.
Next Post Previous Post
Bukobawadau