Bukobawadau

SHEREHE YA ROTARY CLUB; Yafanyika Usiku wa Jana kando ya Ziwa Victoria

Rotary Club Bukoba  lengo lao kubwa ni kujitolea na kujadili masuala muhimu katika nchi zinazoendelea, kuelimishana wenyewe na wadau wanao wazunguka, kujenga uhusiano na mashirika ya kimataifa na miradi ya fedha. 

Pichani baadhi ya wanachama wa Rotary Club kushoto ni Mzee Masabala.
Ni hafla fupi ya kupongezana kwa kufikisha miaka10 ya Jumuia .
 Kutoka kushoto ni mdau Bishanga Egbert na Faisal Kamgisha
Kushoto ni Mdau Mama Matungwa(Mama Warkgarg)
Kushoto ni Bi Betty , Mama Optaty katikati na wa mwisho kulia ni Mdau Teddy Rweyendela.
Mdau Meneja wa CRDB akitoa mawazo yake kwa wanajumuia.
Mbio ndefu zaidi ya mradi walio nao  sasa ni  kukamilika huduma ya maji safi ya kunywa kila sehemu mjini Bukoba
Ingawa Bukoba ni kubwa  kati ya miji wa Tanzania,tayari  maeneo muhimu wameisha kamilisha huduma hiyo.
Wadau waliweza kupata Vyakula aina mbalimbali na Nyama Choma.
Wadau wote kwa pamoja ni wanajumuia wa Rotary Club.
Ikiwa unahitaji kujiunga kama mwanachama wa Club hii  unaweza kuwasiliana na Uongozi wa Warkgard Hotel.
Sehemu ya wadumu katika hafla hii.
Wadau mbalimbali katika hili na lile.
Labda kwa kukumbushia ndg Mdau kiwanja hiki ni kile tulicho wahi kukiongelea juu ya jitiada za Manispaa na swala zima la mazingira hapa ni jirani kabisa na Daraja la Bukoba Club.
Anaonekana mshereheshaji wa Shughuli nzima Mc Msafiri.
Hakika wadau wote walijipanga vyema.
Kila siku za Alhamisi wadau hawa wamekubaliana kuwa wanakutana kwenye Hotel ya Warkgard Annex.
TEMBELEA bukobawadau blogspotspot kwa habari na matukio ya Nyumbani kila Siku.!!!!

Next Post Previous Post
Bukobawadau