Bukobawadau

USAFI WA MAZINGIRA WAZIDI KUIMARIKA PEMBEZONI MWA ZIWA VICTORIA.

Sera ya sheria ya usimamizi wa Mazingira Na. 20 ya mwaka 2004 imeendelea kutekelezwa katika mkoa wa Kagera.Katika utekelezaji wa sera na sheria,Mkoa uliandaa mpango shirikishi jamii wa hifadhi ya mazingira. Mpango huu unaainisha uhusiano uliopo kati ya uharibifu wa mazingira na umaskini uliokithiri kwa sababu maliasili kama vile ardhi,misitu na vyanzo vya maji;ambazo hutumika katika uzalishaji huharibiwa na kushindwa kutoa tija inayokusudiwa na hivyo kukwamisha juhudi za wananchi kufikia lengo la maisha bora kama ilivyo katika Dira ya Taifa ya maendeleo (2025)
Mikakakti ya utekelezaji wa mpango wa hifadhi ya mazingira ya ziwa vixtoria iliyotekelezwa katika kipindi hiki na kutoa Elimu kwa wadau wa ziwa Victoria kwa kupitia semina na makongamano ya wavuvi, viongozi wa Serikali,Viongozi wa asasi zisizo za Kiserikali,wamiliki wa vyombo vya usafiri wa maji,na jamii iliyo kando kando ya ziwa Victoria.
 Taasisi ya uangalizi na uendelezaji wa ziwa Victoria (LVFO) kwa kushirikiana na wadau wengine wa ziwa Victoria wamesaidia kutekeleza mkakati kabambe wa Mkoa wa kuunda na kuwezesha vikundi vya ulinzi wa Rasilimali na usimamizi shirikishi wa Rasilimali ikiwa ni pamoja na dhana ya ujasiriamali na kuinua kipato cha wananchi kwa kutumia ziwa Victoria bila kuathiri mazingira.
Bustani safi zenye Viti vilivyo jengewa pembezoni mwa Ziwa Victoria hakika mazingira yanapendeza.
 Na hii ndio sehemu itakpofanyika Birthday ya Mwaka Mmoja wa Libeneke la Bukobawadau
Manispaa ya Bukoba imefanya utekelezaji wa upandaji na utunzaji miti  pembezoni  mwa ziwa Victoria.
Hali kama hii ya kijana huyu aliye kutwa na Camera yetu amejilaza mchangani/ufukweni Bukobawadau tunaona ni mojawapo ya changamoto kwa Manispaa na wasimamizi au walinzi wa maeneo haya.
Next Post Previous Post
Bukobawadau