Bukobawadau

WADAU TUNAOMBA USHIRIKIANO KATIKA HILI:Mdau mwenzetu anahitaji kujua lolote juu ya email hii.....!!!!!

Mwesiga Alfred mwesialfred@gmail.com


Kaka pole na kazi ngumu za kutujuza mambo kadhaa yajitokezayo mahali
tofauti tofauti.....waitu kasinge muno.
Mdau,nimekuwa nikifuatilia sana blog yetu,naamini wengi watakuwa
wamefaidika kutokana nayo kama mimi nilivyofaidika.

Leo nina shida binafsi kaka.....naishi Dar ambako ndiko natafutia

mkate wangu wa kila siku, sasa kuna bosi wangu wakati tunapiga stori
akanifahamisha kuwa alisoma shule ya Sekondari Bukoba (Bukoba Sec) na
kumaliza mwaka 1972 (japo siyo mzaliwa wa huko)....akanipa kazi (si
unajua bosi anaagiza tu?) akasema kuna mwalimu wake alikuwa rafiki
yake sana, alikuwa anaitwa HILARY MOHAMMED, akadai kuwa alikuwa ni
mwenyeji wa KAMACHUMU, na mwenye asili ya KIARABU; akasema nimsaidie
kutafuta habari zake na iwapo bado yupo au la, au yuko wapi kwa sasa!

Baada ya kazi hiyo ngumu, nikakufikiria wewe mtafiti wa mambo hata

yaliyojificha,nikaona nikuombe unisaidie kwa namna uwezavyo katika
hili ili kwamba kazi ya bosi wangu niikamilishe kwa usahihi.
Natanguliza shukrani kaka.

Bati "Eofisi einamu owawe, eikala ekingwile"; waitu kasinge


Mwesiga Mwesigwa
Next Post Previous Post
Bukobawadau