Bukobawadau

HOJA YA KILIMO KWANZA NA WAKULIMA WA KIGENI


Na E.Sabuni.
Mimi ni mtanzania ninayejivunia utanzania wangu. Naomba kuongelea hili swala la kilimo kwanza. Mimi kama mimi naomna hili swala linapelekwa kisiasa kuliko ilivyotegemewa. Jamani tunaposema kilimo kwanza mara Tenda za matrekta zimeishatoka haraka sana na watu kuanza kuvuna hela isiyokuwa na jasho kwa kutuingizia vitu vibovu kwa kweli inasikitisha sana. Utasemaje kilimo kwanza wakati wakulima wenyewe ujawapa mbinu za hicho kilimo kwanza mnachosema, mtanatangaza kilimo kwanza ndo mfumuko wa bei za vyakula kwanza kweli inasikitisha. Pili kwa nini serikali haikai ikafikiria hivi vitu wanavyofanya vinaenda kunyume na matakwa ya wanainchi? Sawa kilimo kwanza mmeturetea power tiller, power tiller zenyewe vimeo hasa hizi kubwa kwanza mbovu, pili ulaji wa mafuta kupita kiasi kila mtu anazikimbia anaona bora kutumia jembe la mkono kuliko hizo power tiller sijui trekta.

Napenda kuuliza kwanini tuna wataalamu wa kilimo? Wote wamejazana hapa Dar, Arusha, Mwanza  napo ni ofisi za mjini sio vijijini hawataki kwenda mikoa mingine kisa haina maendeleo na miundo mbinu mibovu eti kilimo kwanza kilimo kwanza mjini uliona wapi? Ifike wakati serikali ipeleke wataalamu mikoani hasa ile inayozalisha vyakula kwa wingi sio kuweka watu wa chin indo wanafaa kufanyakazi vijijini wakati wa mijini wanakula posho ambazo hawajazifanyia kazi na kupeana safari za nje ovyo ovyo basi hizo safari wapewe watu wanaofanyakazi mikoani wakajifunze kuliko wanaokaa mini.

Nasikitika kuona Tanzania kuona eti tunamfuko wa bei za vyakula kweli. Mimi binafisi naomba kilimo kwanza neno lifutwe liwe tumbo kwanza. Nimesikia eti serikari ya Marekani wametoa hela kwa ajili ya kilimo kwanza hizo hatutaziona make ndo kwanza zaidi ya kuona matrekta ya mchina yanayowaumiza wananchi yanakula mafuta kama hayana akili nzuri na ubovu kila mara  badala ya kumsaidia mwananchi yana muumiza.


HOJA NYINGINE (WAKULIMA WA KIGENI)
Nikirudi tena kwenye hoja ya wakulima wa kigeni hivi kweli niwakati wake? Mimi naona sio wakati wake naona mnatuletea watu wakuacha wametualibia ardhi yetu na wengine kuzamia moja kwa moja make nchi yetu ni shamba la bibi watu wanachuma na kuondoka. Pili kuwakumbatia wakulima wakigeni na kuwapa ardhi kulima mazao ambayo wakulima wakawaida wakipewa mafunzo watalima kwa utaalamu zaidi. Mfano nasikia kuna wachina wanalima mboga za majani aina zote pale mto Ruvu na ujue wao wanauelewa  wa juu kwa maswala ya kilimo hivi kweli ni haki? Hivi kweli wakulima wadogo wadogo wataweza kupata soko? Make nasikia wanaiginza fuso tatu kila siku pale kariakoo na wameteka mahoteli ya hapa Dar yote  hivi unafikiri sisi umasikini utakakwisha make kila mtu akipata sehemu anataka aibe kwanza. Na hiyo itakuwa dili ya mtu kawaweka hapo anapata 10% yake. Lakini itafika wakati wananchi tutaamua tutawafukuza kwenye ardhi yetu.
Next Post Previous Post
Bukobawadau