Bukobawadau

AJALI YA SEMI-TRELA KATIKATI YA MLIMA WA NYANGOYE HIVI PUNDE!!!!

Ni ajali iliyotokea muda mchache uliopita katikati  ya Mlima "Nyangoye"Hamugembe  mjini hapa.Baada ya gari aina ya SEMI-trela yenye nambari T531BTE likiwa limepakia  mzigo wa Dagaa  tayari kwa safari kuelekea Jijini Mbeya.
 Baada ya kushindwa kupandisha Mlima huu wa Nyangoye, hali iliyopelekea kupinduka.
  Watu waliokuwemo wamenusurika kifo.
Ukubwa wa muinuko na Wingi wa mzigo vimepelekea Gari kurudi nyuma na kupinduka.

 Pichani ni UTINGO wa Gari hili  aliyejitambulisha kama Ndugu  Gilbafasi Daudi Benadi.
Hali ilivyo eneo hili la barabara ya Uganda mlima wa "Nyangoye"
Next Post Previous Post
Bukobawadau