Bukobawadau

HAPA NA PALE NA CAMERA YETU ;WADHAMINI WA GERALDINA ORPHANAGE & EDUCATION CENTER WAKUTANA NA BUKOBAWADAU BLOG.

Langoni mwa United Kingdom Warehouse wauzaji na wasambazaji wa Vifaa mbalimbali,kama meza za maofisini ,viti ,vifaa vya umeme, laptop nk.Na zilipo ofisi za bukobawadau blogspot,waliopo barabara ya Kashozi eneo maharufu kama majinjioni.
Ndani ya United warehouse,zilipo pia ofisi zetu wanakutana na blogger Mc Baraka ,pichani ni Ndg Derek yeye ni volunteer wa (GOEC) "Geraldina Orphanage and Education Center uko nchini  Canada.
 Tumeweza kuongea mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kutekeleza ilani ya mahusiano katika maisha nipo katika kuamini umuhimu wa network,na baada ya hili na lile nimeongozana nao mpaka ofisi ya Mkuu wa Wilaya pia nikaongozana nao ili nipate kujua kile walichokifanya katika kuwasaidia watoto yatima wa kituo cha (GOEC)kilichopo maeneo ya Kyabitembe ndani ya Manispaa ya Bukoba.

Kutoka kushoto ni Ndg Thadeo mkuu wa kituo cha (GOEC)bukoba,wa pili ni Emily ni International Fundrasing Director wa (GOEC) Canada,Mr Derek ni volunteer wa (GOEC)nchini Canada yalipo makao yao na wa mwisho ni Miranda yeye ni Board member na Volunteer wa (GOEC) kwa hapa Bukoba.
Wameweza kuanzisha ujenzi wa Vyumba viwili vya madarasa
Anaitwa Emily pichani akijaribu kile anachokiamini  kwa moyo mmoja  na katika hili  nanukuu alichokisema ;'I am contributing to the Permanent Centre at the future site of Gerladina Orphanage and Education Centre!! (don't be fooled - I contributed much more to the entertainment of the real workmen than any form of construction!!'
Hapa ni shule ya Msingi Nshambya, shule yenye wanafunzi 20 wanaolelewa kwenye kituo cha (GOEC)
Mwalimu Mkuu akisalimiana na Mr Darek na kumkaribisha kwa mara nyingine  kwani majuzi walikuwepo shuleni hapa na shule iliomba msaada wa mipira na vifaa vinginevyo.
 Hisia nilizonazo hapa nashindwa kutoa maelezo!!!!
 Baadhi ya walimu na Wanafunzi wa Shule ya Msingi Nshambya.
 Msaadawa mipira miwili ukikabidhiwa kwa mwalimu wa Michezo
Wanafunzi wakionyesha Mipira wanayochezea kabla ya nehema hii kuwafikia!!
 Changamoto nyingine ni wanafunzi kukalia Nyasi madarasani!!!!
Shule hii pia inatoa mafunzo ya Ufundi.


BUKOBAWADAU BLOG TUNATOA SHUKURANI ZETU ZA DHATI KWA UJUMBE NA VIONGOZI WA GERALDINA ORPHANAGE  KWA KUWASAIDIA WATOTO WAHITAJI!!!



Gonga neno Older post kupata matukio yaliyopita!!!

Moja kati ya vivutio Mjini bukoba ni pamoja na maeneo ya Mlima wa Kashura
Hivi ndivyo alivyo vutiwa Milanda na hapa anachukua picha ya muonekano wa Mji wa Bukoba.
Kama kitu cha kujivunia nawapeleka wakapaone Walk Gard Hotel
Wanakutana na kubadilishana mawazo na Mama Matungwa Mkurugenzi "THE WALKGARD HOTELS AND TOURS"wa pili kulia.
Hakika wamevutiwa sana na mwonekano na mazingira ya hotel hii.
Hotel ipo kileleni mwa Mlima Kashura na usawa wa Ziwa Victoria ,Utalii ni mojawapo ya shughuli zao na sasa tumekamilika na Wizara ya Utalii  ina Mdau...!!! 
 Sehemu mbalimbali katika hotel ya Walk Gard
Camera  ya hapa na pale Mpaka Chumbani!!!!
 

MUHIMU;TUNAOMBA KUTUSHIRIKISHA KATIKA TUKIO LOLOTE ,SEHEMU YOYOTE NA KUTUTUMIA HABARI,VISA VYA KIMAISHA, CHANGAMOTO ZA KIMAENDELEO  NA KUTUPA USHAURI PIA WAWEZA KUTANGAZA NASI BIASHARA YAKO, MPAKA HIVI SASA ZAIDI YA WATU 3000 UTEMBELEA TOVUTI YETU KILA SIKU!!!!

Next Post Previous Post
Bukobawadau