Bukobawadau

KONGAMANO LA WANAFUNZI WA KIISLAM MKOANI KAGERA JUU YA YA HUJUMA YA MATOKEO YA KIDATO CHA SITA MWAKA 2011/2012 KWA WANAFUNZI WA KIISLAM.

Sheikh Haruna Kichwabuta akitoa nasaha juu ya tamko la waislam wa mkoa wa kagera kuhusu hujuma ya matokeo ya kidato cha sita mwaka 2011/2012 kwa wanafunzi wa kiislam.
Baadhi ya wanafunzi wa kiislam waliojitokeza katika kongamano hii leo 17/6/2012 katika viwanja vya shule ya msingi jamia.
Anaonekana Ustaadh Said Zuberi Bamanya akitoa mada juu ya hali halisi ya vijana wa kiislam shuleni,hakizao na nafasi ya wazazi .
 Wadau mbalimbali wakifuatilia Kongamano linavyo endelea, wa mbele mkuu wa Shule ya Kiislam  Jamia Ajath Nulia Nuru.
 Wanafunzi wakifuatilia   MANENO  ya Maustaadh na kuyajengea hoja papo kwa papo.
Wazee nao wameshiriki kikamilifu.
Imam Hamza pichani akibabadua juu ya matukio malimbali yaliyopita na mafunzo yake.
Uislamu ni dini ya U shujaa na ujanadume kasikika akitamka kwa hisiabUstaadh Othman.
 Mwendeshaji na mshereheshaji Ustaadh  Masoud Hussein.
Kabla ya majumuisho Ustaadh Mikidadi  Mbaruku alifafanua juu mfumo mzima wa Baraza la mitihani (NECTA)na utendaji kazi wake.
Amir Tamsya  namaanisha  (mwenyekiti wa jumuiya ya wanafunzi na vijana wa kiislam Tanzania Mkoa wa Kagera)  Ustaadh Mzamil Twahir  akitoa TAMKO juu ya  hujuma ya matokeo ya kidato cha sita  mwaka 2011/2012 kwa ufupi amesema: amesema;.
  • Wanaunga mkono matamko yote ya Waislamu yaliokwisha toleo kuhusu hujuma dhidi ya Wanafunzi wa Kiislam.
  • Wanaunga Mkono tarifa ya Mufti wa Tanzania, Sheikh Issa Shaban Bin Simba kwa vyombo vya habari aliyoitoa tarehe 6/6/2012 Jijini Tanga.
  • Uchunguzi wa kina ufanyike kwa masomo yote kwa miaka kumi iliyopita.
  • Bila uchunguzi kufanyika watawashawishi wanafunzi wa Kiislam wasifanyen Mtihani wowote unao andalwa na Baraza la mitihani Tanzania(Necta)
  • wanataka wafanyakazi wote wa Baraza la Mitihani wawajibishwe, baraza liundwe upya na pawepo na Uwiano sawa  kwa dini zote.
Next Post Previous Post
Bukobawadau