SHULE YA WASICHANA YA SEKONDARI YA RUTH MSAFIRI
Na, Judith Blasio
Cha mno chunga sana jasho la mtu binafsi likienda bwelele bila hata hata ahsante -wapendwa wazalendo wanakijiji hapo hakuna baraka kabisa.
Shule kukabidhiwa kwa wananchi ni vita na viini macho vya kisiasa.
Adhaniaye amesimama na angalia sana asi.....................
Oh nampa pole sana mh mbunge aliyemaliza muda wake na kumfariji
kuwa uwe mpole sana katika hili na usikwazwe. Wewe hi mwanamaombi
liombee hili na songa mbele utauona mkono wa bwana.
Wananchi wa katoke nawapeni pole kwa kutwishwa mzigo na wachache
wenu wanadiriki kutumia kivuli cha jamii kutenda unyama bila aibu wala
woga. Kiumbe usimwogope binadamu lakini mwogope Mungu.
Cha mno chunga sana jasho la mtu binafsi likienda bwelele bila hata hata ahsante -wapendwa wazalendo wanakijiji hapo hakuna baraka kabisa.
Mwalimu mwenzagu mheshimiwa mkuu ngoma ilinoga lakini fuatilia sana
kwa kina ukweli haujajua na tafadhali ukiujua ukweli usione aibu
kutueleza.
Kaka yangu mh diwani wa katoke wewe wajua kilicho ndani ya moyo
wako pengine utatuzi usio na washangiliaji ungefaa zaidi kwani wacheza
ngoma wanacheza mlio wa ngoma bila kujua kilicho ndani ya ngoma.
Bukoba wadau mimi hayo ndio machache yangu kama mwana kijiji na ndugu wa damu.
Na,Judith Blasio
judblasio@yahoo.co.uk