Bukobawadau

USIKU WA VALENTINE BUKOBA,WALKGARD ANNEX KWALIPUKA SHANGWE ILE MBAYA!!

 Ni taswira ya usiku wa  wapendanao (Valentine Special Party) ilivyoweza kufana ile mbaya ndani ya Hotel ya Walkgard Annex na kuhudhuliwa na watu kibao,ambapo zaidi ya wapendanao 300 wamejitokeza na kuweza kuupamba vyema ukumbi huu na kufanya usiku huo kuonekana kivingine zaidi..

 Taswira ya kaunta ndani ya Walkgard Annex Hotel.
Mkurugenzi wa Walkgard Annex mama Adventina Matungwa akifungua rasmi shughuli hii.Mama huyu anakua mfano wa ni vipi mtu utoke kwa siku kama hii,kwa upendo mkubwa mama huyu ananing'ata sikio kuwa asilimia 20 ya mapato ya siku hii(yaani faida yake) anawapa kituo cha Radio cha Kasibante wakiwakilishe kwa watoto yatima na waishio kwenye mazingira magumu.
 kaka Mkubwa Ernest Nyambo ambaye hapo anasimama kama mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya shughuli hiyo,hakika jamaa huyu amekuwa kimbilio la wengi kwenye mengi,hapo akiwashukuru wadau waliojitokeza kwa wingi pia akiwaomba ushirikiano wa pamoja kufanya shangwe inoge
 Mzee Mchuluza akishow love na familia yake.
Mdau Alley Simba na mkewe na mdada ambaye ni mgeni machoni mwetu,ila  shughuli yake daahh!!
Mdau Mr Phocas mzee wa Equilizer na mkewe.
Hivi ndivyo ilivyo wakirisha familia ya Ndg Mganyizi Zachwa.
Wanaonekana wanadada pichani kutoka kushote Bi Salome chui na London,Bi Lilian Peter Mwise na Bi Maua Ramadhani.
Mr na Mrs Patrick pombe walikuwepo.
 Hakika watu wameweza kuitikia.
 Kwa mtambo akiwa amesimama Dj Mkongwe katika tasnia hii ya burudani, na upande wa Mc's mshereheshaji wa shughuli hii Bi Joyce Lubozi  pichani (kushoto)alihusika na kumudu vyema.
Watu walivyo enea vyema ukumbini.
Sura ngeni na mikato ya kisasa ndio ulikuwa mpango mzima hiyo jana

Mdau Fide akiwakilisha kwa mbwembwe upendo wake ila kubwa zaidi ni vile alivyoichukulia siku hii kaipa heshima yake kwa kuwa smart ile mbaya na utulivu mkubwa
 Mr & Mrs Deo Rugaibura,kaka yetu huyu na familia yake ni mfano wa kuigwa,jamaa anaishi kama yupo majuu,upendo na pia anajuwa kupangilia vitu,walipendeza sana hawa wadau,BIG UP KAKA DEO 
 Meza ya familia ya Mama Muhazi,Mama yetu huyu anastahili tuzo ya heshima maana naye ni mfano wa kuigwa,ni mama mpambanaji hasa,mengi zaidi nitafute pembeni,HESHIMA YAKO MAMA
Kushoto ni mwanadada Devotha kama ilivyo kawaida kutunisha mambo flani, pembeni ni Mwanadada jina kapuni kwa maelekezo tuliyopewa.
Kama hawa ndio walikuwa sehemu ya walengwa,eeeh maana kujizeesha na kujiweka nyumbani mwaka hadi mwaka sio mambo,asante sana Mzee wetu Stanford na familia yako kwa kuunga mkono juhudi za waandaaji
 Kutoka na familia ndilo jambo tunahimiza sana pale nafasi inapokuwepo,asante Mzee Mushobozi
 Jopo likiendelea na mchakato wa kutafuta washindi kwa usiku huu.
Burudani ikiendelea chini ya Dj Max
Wadada hawa pia ni muhimu sana katika jamii maana ni wa kileo wasio na zengwe na mtu yoyote,wanadai raha jipe mwenyewe ikibidi,safi sana dada Rehema,Devota na bi Maua Ramadhani
 Burudani imeshika kasi,namuona Super Mkude akisakata na mwanae Mainda pembeni Jumanne Bingwa,Mrs Mohamed Kassim kwa mbali Mrs Mkude wakionesha furaha sana kwa kucheza muziki.
Watu wakishow love ni changanikeni wanaume, wanawake, wapenzi mle mle,kaka, dada,baba, na mama zao
 Furaha yote hii inaletwa kwako na www.bukobawadau.blogspot.com.
Hapa ninachoweza kusema ni kwamba Wamjini utawajua tu!!
 Wana wa kikwemu pichani anaonekana Bi Jamila na Bi Zena.
Mdau Jamal Kalumuna na familia yake,Big up sana Jamco.
 Ulifika wakati wa zawadi,kamati na uongozi uliandaa zawadi kwa pea yaani watu wawili wawili, lengo likiwa kutoa zawadi kifamilia zaidi iliposhindikana ilibidi kutazama wale waliopendeza sana na kuvalia ki VALENTINE zaidi na pia zawadi zilitengwa kwa kuzingatia Umri, Pichani ni washindi kwa UMRI wa miaka 35 kushuka chini Dada Lilian na Da Mainda

Hapo ni washindi kwa shindano la wale wa miaka 35 mpaka 45 nao ni Mrs Agneta Kalike na Mrs Gode Bayona,hakika walikuwa wamewaka na mchakato wa kupata washindi ulikuwa wa uhuru na haki kabisa,savuu kwenu wanamama.
 Zawadi ya mwisho ilikuwa ya shindano kwa wenye miaka 45 na kuendelea,ndipo meneja wetu Mr Mushobozi na mke wake wakaibuka washindi,hakika walikuwa kifamilia zaidi pozi zao,umakini na kupendeza viliwapa ushindi,pichani wakipokea zawadi kutoka kwa Afisa utamaduni Mr.Rugeiyamu
 Ushindi ni raha jamani,hapo washindi wameungana na watoto wao kupata picha ya pamoja na wazazi wao, kwa msisitizo zaidi WALKGARD wametoa zawadi pia na CHETI kwa washindi na kusema ni vyema ukitunze maana ni sehemu ya CV zakooooo aaaaah aaaah aaaaah huwezi kujuwa kuna leo na kesho
Taswira kuelekea ukumbini
Nyama choma   yenye ladha nzuri,wahaya wanasema (eshaile)Siku zote unapo ongelea Walkgard ni sawa na kuongelea kile chenye ubora.
 Mama Mick akibadilishana mawazo na mdau mwenzake
 Shuguli ni watu kula  kunywa na kufurahi

 Mdau Muhamed Kassim naye ndani.
 Mwanadada Lilian Peter.
BUKOBAWADAU TUMEFURAHISHWA SANA NA SHUGHULI HII TANGU ZOEZI ZIMA LIMEANZA MPAKA MWISHO ATUKUAMINI NAMNA WATU WALIVYOKUWA WANANUNUA MEZA KABLA YA SIKU NA WALIVYOJITOKEZA KWA WINGI HUKU WAKIWA WAMEPENDEZA KWA KUTUPIA/KUNYUKA  PAMBA KALI!!!
Mzee Sadi Idd na Mdau Top mzee wa balo.
Mdau kila chenye mwanzo hakikosi kuwa na mwisho, huu ndio mwisho wa taswira ndani ya WALKGARD ANNEX kwa usiku wa wapendanao,baada ya hapo libeneke letu likaendelea ndani ya kisima  ndani cha burudani  ndani ya Club linaz matukio ya zaidi utayapata kupitia facebook page yetu.
Next Post Previous Post
Bukobawadau