Bukobawadau

MKASA WA KUOTA NDEVU KWA MWANAMAMA MARIAM

Mariam,mwanamke aliyezaliwa nchini Ujerumani amepatwa na mkasa wa kuota ndevu nyingi kama mwanaume.Awali alikuwa akiziondoa ndevu hizo kwa njia mbalimbali lakini ilipofika mwaka 2008 aliamua kuachana na vifaa vyote vya kuondolea ndevu na kuacha ndevu hizo zikue ambapo kwa madai yake,baada ya kuziachia ndevu hizo anajisikia kujiamini zaidi kuliko kipindi alichokuwa akiziondoa.Tatizo hilo la kuota ndevu mithili ya mwanaume alilipata miaka 28 iliyopita mara tu baada ya kujifugua mtoto wake wa kwanza.Majaribio mbalimbali ya kimaabara yamefanyika ili kuona ni sababu zipi zinazomfanya mwanamke huyo kuota ndevu nyingi kiasi hicho lakini mapaka sasa hakuna kilichogundulika.
Next Post Previous Post
Bukobawadau