Bukobawadau

TUWAKUMBUKE WATOTO WENYE MTINDIO WA UBONGO KAMA KUNDI MAALUM KATIKA JAMII ZETU

 Stephanie Koster Mama Mlezi wa Kituo cha Mt. Nicholaus Children Center Akisoma Historia ya Kituo Kwa Wageni Waliotembelea Kituo hapo tarehe 05/02/2013

Mwanadamu mkamilifu apoamka asubuhi na kuanza siku yake kwa kutekeleza majukumu yake ya kawaida ya kila siku ya kujiingizia kipato halali cha kujikimu na kuyafanya maisha yasonge mbele huwa siyo rahisi kukumbuka kuwa kuna binadamu ambao wanahitaji msaada na uangalizi wa karibu sana.

Mashirika, Taasisi mbalimbali za serikali na binafsi aidha watu mmoja mmoja katika kuangalia makundi maalum ya kusaidia mara nyingi huwakumbuka watoto yatima na waishio katika mazingira magumu, wazee na walemavu wa viungo. Lakini kuna kundi maalum ambalo jamii hulisahau bila kulipa kipaumbele..
Walemavu wenye utindio wa ubongo katika jamii zetu za kitanzania husaulika sana na kuachwa bila msaada wowote wa karibu, mfano kupatiwa huduma ya karibu kama huduma za kiafya, elimu aidha kuwa na mahusiano ya kawaida katika jamii zetu.
Familia zilizo nyingi pamoja na jamii zetu akizaliwa mtoto mwenye utindio wa ubongo huonekana kuwa ni mkosi katika familia jambo ambalo hupelekea mtoto huyo kutengwa au kufichwa ndani au kujengewa kijumba mbali na familia na kunyimwa haki zake za msingi kama watoto wengine.
Lakini kutokana na kundi hilo hitaji kuonekana halina msaada wowote, mfano vituo maalum vya kuwalelea watoto hao na kuwapatia mahitaji yao maalum ikiwemo  elimu, aidha kutokana kuwa katika  jamii watoto hao wapo wengi na hawana msaada Mama Stephanie Koster aliamua kuanzisha kituo cha kuwalea watoto hao.
Stephanie Koster ni mama wa Kijerumani ambaye aliliona tatizo hilo  katika mkoa wa Kagera na kuamua kuanzisha kituo cha kuwalea watoto wenye ulemavu wa mtindio wa ubongo chini ya kanisa Katoriki Jimbo la Bukoba katika eneo la Kemondo Wilaya ya Bukoba na kituo kinaitwa Mt. Nicholaus.
Mama Koster ana upendo mkubwa na watoto hao na anajitoa kuwapenda, kuwalea, kuwatunza na   kuwapatia huduma za afya na elimu na kuwafanya watoto hao   kujisikia wanadamu kama wengine kwani mama huyo huwapeleka watoto hao katika shule za karibu za Mubembe na Bethania.
Mama Koster mama Mjerumani anasema kituo hicho kiliazishwa na kufunguliwa rasmi tarehe 13.11.2011 na Mhashamu Askofu Nestory Timanywa  Askofu jimbo la Bukoba wakati huo na kituo hicho kilianza na watoto kumi wakiwa chini ya mama huyo mlezi na kina uwezo wa watoto 25.
Stephanie Koster anasema alianzisha kituo hicho ili kuionyesha jamii kuwa watoto hao wana haki sawa na wengine katika jamii na wazazi wenye watoto hao wanapaswa kuwalea watoto wenyewe bila ya kuona kuwa huo ni mkosi au kuwatenga.
“Ni watoto ambao hawawezi kusaidiwa na familia ndiyo wanapokelewa katika kituo hiki cha Mt. Nicholaus na kwa mtizamo huo, maombi hupelekwa kwa kupitia  ofisi za ustawi wa jamii kabla ya kupokelewa kituoni.” Alifafanua mama Koster.
Wito kwa jamii, mama Koster anatoa wito kwa jamii ya watanzania  kujitolea kuwahudumia watoto hao kwani kituo hicho hupokea watu wa kujitolea “Volunteers”  kutoka nje ya nchi kama Ujerumani na wengine hutoka katika jamii ya kitanzania walio na elimu ya malezi ya watoto.
Shukrani, Stephanie Koster mama mlezi wa kituo cha Mt. Nicholaus anatoa shukrani zake za dhati  kwa Familia ya Katibu Tawala Mkoa Kagera Bw. Nassor Mnambira pamoja na rafiki wa familia yake kufika kituoni hapo  na kutoa zawadi kwa watoto hao pia na wote wanaoendelea kufika na kutoa misaada mbalimbali kwa watoto . “Toa ulichachoa na Bwana atakuongezea
 Watoto Wenye Mtindio wa Ubongo Wakiimba na Kufurahi Mbele ya Wageni Waliowatembelea (Hawapo Pichani)
 Watoto Wenye Ulemavu Pia na Wageni Waliofika Kuwaona Kituoni Kwao.
 Mama Mnambira Akitoa Zawadi zake Kwa Mama Mlezi wa Kituo
 Huyu ni Mmmoja wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo
Huyu ni Mmmoja wa Watoto Wenye Ulemavu wa Mtindio wa Ubongo
Mtoto Huyu Ana Tatizo la Ugonjwa Ngozi Lakini Kabla ya Kuletwa Kituoni Wazazi wake na Jamii Ilimtenga kwa Kumjengea Kijumba Chake Mwenyewe na Aliishi Peke  Yake, Lakini Sasa Anajumuika na Watoto Wenziwe.
 Mke wa Katibu Tawala Mkoa Kagera Mama Mnambira Akionyesha Upendo Kwa Mtoto Huyu Kwa Kumgongea na Kinywaji Chake.
 Pia Ujumbe Kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Kagera Ulikuwepo Katika Kutoa Chochote kwa Watoto hao wahitaji
 Picha ya Baada ya Kufurahia

Imeandliwa na:
Sylvester Raphael
AFISA HABARI MKOA
KAGERA @ 2013
Next Post Previous Post
Bukobawadau