Bukobawadau

B0TI YAZAMA ,YAUA WATANO

 WAFANYABIASHARA watano wamekufa maji baada ya boti waliyokuwa wakisafiria ya Mv. Kitoko2 kuzama kwenye Ziwa Victoria kwa madai ya kuzidisha uzito.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, George Mayunga, alikiri kutokea kwa ajali hiyo Mei 23, 2014 saa nane usiku baada ya injini ya boti hiyo kuzima ghafla ikiwa safarini.
Alisema boti hiyo ilikuwa ikitoka Bugombe kupitia Kasenye kuelekea Mganza na abiria watano, kati yao mwili wa Jane Mlekatete (36) raia wa Rwanda uliopolewa.
Aliwataja wengine waliokuwepo kwenye boti hiyo kuwa ni Chikola Filbert (22) na Mapinduzi Daud (38), wengine walitambuliwa kwa jina moja ambao ni Asha na Suzy.
Next Post Previous Post
Bukobawadau