MKUU wa Wilaya ya Karagwe mkoani Kagera, Darry Rwegasira amepata
ajali katika Kijiji cha Kalebezo, Kata ya Nyamirembe Wilayani Chato
mkoani Geita juzi.
Akizungumza kwa njia ya simu na Tanzania Daima, Mkuu wa Mkoa wa
Geita, Said Magalula, alisema Rwegasira alipata ajali hiyo akiwa na
gari namba STK 3768 akiwa safari kuelekea wilayani Sengerema mkoani
Mwanza.
Magalula alisema chanzo cha ajali hiyo ni hatua ya dereva Said Adamu
(59), kujaribu kumkwepa mtoto Jonas Tyson (7) ambaye alikatisha ghafla
barabarani na kusababisha gari kupinduka na kuharibika vibaya.
Hata hivyo, katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha na hali za majeruhi akiwemo mkuu huyo wa wilaya zinaendelea vizuri.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comment:
Post a Comment