Bukobawadau

CHECK VIDEO JLO ABADILI MAWAZO, ATASHIRIKI UFUNGUZI WA KOMBE LA DUNIA KESHO

Mwanamuziki kutoka nchini Marekani Jennifer Lopez amebadili msimammo wa kutohudhuria sherehe za ufunguzi wa fainali za kombe la dunia, na kutangaza kuwa atakuwa sehemu ya sherehe hizo zitakazofanyika kesho huko Arena de São Paulo, mjini São Paulo.

J-Lo ambae hakutoa sababu za kutohudhuria sherehe hizo siku mbili zilizopita, amesema ameona kuna umuhimu wa kuhudhuria katika sherehe za ufunguzi hivyo hii leo usiku anatarajia kusafiri kuelekea nchini Brazil.
.Amesema anaamini mashabiki wake walisikitishwa na taarifa ambazo zilitolewa na shirikisho la soka dunia FIFA za kutokuwa sehemu ya sherehe hizo hapo kesho, hivyo ameona sio jambo jema kufanya hivyo kwa kuhisi huenda akawanyima haki wanaompenda kumuona akiwa jukwaani sambamba na wasanii wengine, ambapo wataimba wimbo maalum wa kombe la dunia wa mwaka huu unaoitwa ‘We Are One’
Wasanii wengine watakaoshirikiana na Jennifer Lopez kuimba wimbo huo ni Pitbull na mwenyeji Claudia Leitte.
 Check video hapa Chini-We Are One (Ole Ola) [The Official 2014 FIFA World Cup Song] 
Next Post Previous Post
Bukobawadau