Bukobawadau

SERIKALI YAPIGA 'STOP' UVUTAJI WA SHISHA

Uvitaji wa Shisha ni sawa na uvutaji wa sigara kulingana na madaktari
Serikali ya Tanzania imepiga marufuku uvutaji wa Shisha.
Uraibu huo unaohusisha uvutaji wa Tumbaku yenye ladha tofauti tofauti ambayo hutiwa ndani ya chupa kubwa na kuvutwa kwa mirija, umeshika kasi sana Tanzania hasa miongoni mwa vijana wadogo mjini Dar Es Salaam.
 Baadhi ya watu wanaiona Shisha kama isiyokuwa na madhara ya kiafya ikilinganishwa na uvutaji wa Sigara.
Lakini wataalamu wanaamini kuwa uvutaji wa Shisha kwa muda wa saa moja ni sawa na kuvuta sigara miamoja.
Madaktari walitoa onyo kuhusu uvutaji wa Shisha wanakabiliwa na tisho la kuugua Saratani sawa na hatari inayowakabili wavitaji wa sigara.
Next Post Previous Post
Bukobawadau