Bukobawadau

WAZIRI KAMANI AWAASA WANANCHI WA KAGERA KUTUMIA FURSA NZURI ZILIZOPO KUFUGA KISASA ILI KUINUA UCHUMI WA NCHI

  Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Dk. Titus Kamani wa pili kutoka kulia akipata maelezo jinsi ya kuchakata samaki kutoka kwa mchakataji katika kiwanda cha Vicfish Manispaa ya Bukoba
 Waziri Dk. Kamani Akipata Maelezo Jinsi ya Kuandaa na Kukausha Mabaki ya Samaki (Mapanki) Kutoka kwa Mama Kalega Mmiliki wa Kiwanda cha Mapanki Kilichopo Kemondo Lwagati
 Shehena ya Mabaki ya Samaki (Mapanki) yaliyokaushwa Tayari kwa Kusafirishwa Kwenda sokoni
 Mwekezaji Bw. David James Akitoa Maelezo Mbele ya Waziri Kamani Jinsi Alivyojipanga Kuwekeza Katika Sekta ya Mifugo Hasa Ng'ombe na Kujenga Kiwanda cha Kuchinja na Kusindika Nyama Katika Ranchi ya Mabale Wilayani Missenyi
 Waziri Kamani Akiongea na Wananchi Eneo la Kihanga Wilayani Karagwe
 Waziri Dk. Titus Kamani Akiwa Katika Picha ya Pamoja na Wanafunzi wa Chuo cha Mifugo kilichofunguliwa Hivi Karibuni Kikulula Wilayani Karagwe
 Hawa ni Ng'ombe wa Mwaka Mmoja na Nusu Ambapo Wananchi Wameshauriwa kufuga Namna Hii na kuachana na Makundi Makubwa ya Ng'ombe yanayoleta Migogoro Kwenye jamii
 Waziri Kamani Akikagua Kiwanda cha Kusindika minofu ya Samaki Kagera Fish Kemondo.
 Waziri Dk. Kamani Akiangalia Samaki Aina ya Kambale Wanaofugwa Kwenye Mabwawa Katika Eneo la Ruhanga Wilayani Muleba
 Waziri Kamani Akikagua Mabwawa ya Samaki Ruhanga Wilayani Muleba.
Wananchi wa mkoa wa Kagera wameaswa kutumia fursa ya hali ya hewa nzuri,  ardhi nzuri  na upatikanaji wa maji  kwa wingi  katika sehemu mbalimabali za mkoa kuanzisha ufugaji wa kisasa wa mifugo  hasa ng’ombe na samaki katika mabwawa  ili kuinua hali ya uchumi wa wananchi.
Ushauri huo ulitolewa na Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi Mhe. Titus Mlengeya Kamani alipofanya ziara mkoani Kagera kuanzia tarehe 9-11/06/2014. Mhe. Kamani alitoa wito kwa Idara na kitengo cha doria mkoani Kagera kuimarisha doria na kuzuia uvuvi haramu.
Mhe. Kamani alisistiza viongozi wa idara hiyo kutoa elimu kwa wananchi kuhusu ufugaji wa samaki katika mabwawa ili kutoa fursa ya samaki katika ziwa Victoria kuzaliana zaidi. Ushauri huo aliutoa alipotembelea ofisi za uvuvi katika Manispaa ya Bukoba eneo la Custom Karibu na bandari ya Bukoba.
Pia Mhe. Kamani alihaidi kuwa serikali itaendelea kutoa ushirikiano na msaada  wa kitaalam kwa wawekezaji ambao wanajishughulisha katika sekta za viwanada vya kuchakata na kusindika samaki  mara baada ya kutembelea  viwanda vya Vicfish, Kagera Fish na Mapanki Company Limited.
Aidha Mhe. Kamani akiwa Kianga Wilayani Karagwe alitoa wito kwa wananchi wa mkoa wa Kagera kutumia fursa iliyopo ya hali nzuri ya hewa, maji na ardhi kuanzisha ufugaji wa kisasa  hasa ng’ombe na kuachana na migogoro kati ya wakulima na wafugaji ya kupigania ardhi mara kwa mara .
Waziri Kamani alisema serikali itawanyanganya vitalu wawekezaji wote waliopewa vitalu hivyo na wao kuvikodisha kwa wafugaji kutoka nje ya nchi bila kuvitumia wao wenyewe. “Ardhi ya Tanzania ni mali ya watanzania tu na siyo watu toka nje ya nchi.” Alististiza Waziri Kamani.
Vilevile Waziri Kamani aliwahakikishia wananchi kuwa wizara yake imejipanga  kuhakikisha inamaliza migogoro ya wakulima na wafugaji ili sekta ya mifugo iweze kukuza uchumi wa nchi kwa kuvutia wawekezaji kuwekeza kwa wingi katika sekta hiyo.
Akitembelea ranchi za Kikulula Karagwe na Kagoma Muleba na kuongea na wawekezaji waliowekeza katika vitalu vinavyopatikana katika ranchi hizo alisema wanatakiwa kundeleza vitalu vyao na kufuga ufuji wa kisasa ili kukidhi mahitaji ya nyama katika masoko ya ndani na nje ya nchi.
Tayari kuna mwekezaji ambaye anajenga kiwanda cha kusindika nyama katika ranchi ya Mabale Wilayani Missenyi na kiwanda hicho mara baada ya kukamilika kitakuwa kinachinja ng’ombe 300 kwa siku na kusindika ngozi kwa ajili ya bidhaa mbalimbali zitonanazo na ngozi hizo.
Waziri Kamani pia alisema serikali inakusudia kukiboresha chuo cha mifugo ambacho kimeanzishwa cha Kikulula Wilayani Karagwe na kukifanya kuwa Chuo cha Kisasa nchini kwani bado kina fursa kubwa ya ardhi.
Mhe. Kamani akiwa chuoni hapo alisema, “Tanzania vyuo vya mifugo vipo saba tu, na kwasasa taifa linahitaji wagani wa mifugo17000 waliopo ni 5000 tu, vyuo vinazalisha wagani 2500 tu, kwa hiyo chuo hiki kikiboreshewa miundombinu kitaweza kudahili wanafunzi wengi zaidi.”
Imeandaliwa na:
Sylvester Raphael
AFISA HABARI
RS-KAGERA@2014


 
 
Next Post Previous Post
Bukobawadau