Bukobawadau

FANYA KUPITIA KISA HIKI KAMA TULIVYO KIPOKEA.

Fanya kupitia Stori hii inayomhusu jamaa pichani kushoto.
Kuna incident imetokea maeneo ya sinza naomba niwarushie kama ilivyo ili tujifunze kitu
leo asubuhi wamekuja watu 6nyumbani wakasema wanatoka tanesco wamekuja kucheki mita ya luku.wakakorokocha wakasema mita imechezewa kwa hiyo wanakata umeme na kung'oa mita, eti waliona kwenye gps yao kuwa umeme hauendi vema.macho yakatutoka,wakasema fidia na kurudisha umeme kiofisi ni milioni 8! ila tukiwapa milioni 2 wataturudishia.nikawauliza kama mita imechezewa mbona tunanunua umemewa laki 3 kwa mwezi?si ingepaswa tulipe kidogo?wakasema wakati mwingine wakiweka hiyo resistance (eti ndo kifaa cha kuiba umeme) huwa kinafyatuka halaf umeme unakwenda zaidi! wakakata umeme

wakaondoka,tujipange.tujadiliana na mzee tukapata mashaka maana walikuwa wakali halaf wanalazimisha mambo,wamevaa vitambulisho lakini wamevigeuza kwahiyo havisomeki.tukapiga simu tanesco kuwauliza wakasema hao ni vishoka tuite polisi.basi tukawapigia simu waje wachukue laki tano waturudishie umeme,mengine j3. wakaja fasta2 wakarudisha umeme.nikawaambia naenda ATM wasubiri.nikawaacha na mzee.nikatoka mbio mpaka polisi chuo nikawahadithia wakanipa polisi 3 nikaja nao home,tukawakuta wameondoka.mzee akawapigia simu waje hela imepatikana.wakasema tukutane mlimani city,tukafanikiwa kukamata mmoja wengine wakakimbia.tumemuacha selo,tukaandikisha maelezo.tunasubiri hatua itakayofuata.hiyo picha ndo huyo tuliyemkamata!  NDUGU WADAU KUWENI MAKINI NA UTAPELI WA AINA HII!!
Next Post Previous Post
Bukobawadau