Bukobawadau

FULL-TIME: FRANCE 0-1 GERMANY

Bila shaka wala wasiwasi ndivyo anavyo onekana shabiki wa Ujerumani muda mchache kabla ya mchezo wa Robo fainali ya kwanza ya Kombe la dunia ndani ya Maracana. 
Timu ya Ufaransa ilivuka hatua ya 16 baada ya kuwashinda Nigeria kwa 2-0 .
Ujerumani wamepata bao lao  kupitia kwa mchezaji Mats Hummels aliyeweza kujipinda kwa kichwa katika mazingira tata na kuifanya timu yake kuongoza.
Ujerumani wameweza kulinda heshima kwa wepesi tofauti na mechi yao ya hatua ya 16 dhidi ya Argeria baada ya kupata ushindi wa 2-1 katika muda wa ziada wa dakika 120.
Timu zote mbili zikiwa  zimejipanga, matumbo joto kwa ajili ya mchezo wa robo fainali ya kwanza ya Kombe la dunia.
Timu zote mbili zinasimama katika bango lenye ujumbe wa kupinga ubaguzi wa rangi. 
 Mshambuliaji wa Ufaransa Karim Benzema (kushoto) akisalimiana na Mchezaji wa Ujerumani Mesut Ozil - ambaye zamani walikipiga wote katika timu ya Real Madrid 
 Beki waUjerumani Mats Hummels akishangilia bao lake dhidi ya Ufaransa
Ni bao safi la Ujerumani kufuatia kichwa cha Mchezaji Mats Hummels na kumuacha kipa wa Ufaransa  Hugo Lloris hana la kufanya.
Raphael Varane anauacha mpira na kutua kichwani kwa mfungaji Mats Hummels
Anaokoa mpira Kipa wa Ujerumani Manuel Neuer  (kushoto) mbele ya mshambulia wa Ufaransa Karim Benzema 
Mazingira tata pale mchezaji Mathieu Debuchy wa Ufaransa anapo mlima Miroslav Klose wa Ujerumani na kuanguka chini ndani ya eneo la hatari
Kipa wa Ufaransa  Hugo lloris anadaka mpira mbele ya mchezaji wa timu yake mat Patrice Evra (katikati)na Mshambuliaji waUjerumani  mwenye uchu wa mabao Thomas Muller 
Kkipa WA  Ujerumani Manuel Neuer (kulia) akiruka sawia kupangua mpira wa hatari kufuatia kazi nzuri ya Mchezaji Karim Benzema,ambaye kwa siku ya leo hakuonyesha umakini kabisa .
 Mshambuliaji wa Ujerumani  Thomas Mueller (kushoto) akiachia shuti linalo zuiwa na Mlinsi wa Ufaransasa Mamadou Sakho  mnamo dakika ya 85 ya kipindi cha pili
Next Post Previous Post
Bukobawadau