Bukobawadau

UMATI WA WATU WASHIRIKI MAZISHI YA MAREHEMU BI THERESIA KOKWIKIRIZA LAURENT KIJIJINI BUKABUYE -JANA AUG 25,2014

Marehemu  Ma Theresia Kokwikiriza Laurent  enzi za uhai wake 1924-2014
 Marehemu Bi Theresia Kokwikiriza Laurent alizaliwa katika Kijiji BUHEKERA kata ya Bwanjai-Kiziba mnamo June 1924(mwaka elfu moja mia tisa Ishirini na nne.)
 Kifo cha Marehemu Mpendwa Bi Theresia kilitokea siku ya jumamosi Aug 23,2014 katika hospital ya Mkoa Kagera alipokuwa amelazwa kwa siku tatu kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wa Marelia na Uvimbe.
Ndugu Beneth,mjukuu wa Marehemu Bi Theresia akisoma wasifu wa Marehemu.
 Padre akiongoza ibada ya mazishi ya Marehemu Ma Theresea yaliyofanyika nyumbani kwake Kijijini Bukabuye- Katunga siku ya Jana Jumatatu Aug,25,2014
Mwl.Kagirwa ,pichani kushoto ambaye ni Mtoto Mkubwa wa Marehemu na mkuu wa familia.
 Sehemu ya Waombolezaji wakiwa katika ibada ya kuuombea mwili wa Ma Theresia Laurent
Padre akiendelea kutoa mahubili wakati wa ibada ya mazishi
Sehemu ya wananchi na wakazi wa Kijiji cha Bukabuye  ambao wameungana na ndugu, jamaa na marafiki kumsindikiza marehemu Ma Theresia Kokwikiriza Laurent.
Umati wa waombolezaji ukishiriki katika Ibada ya mazishi.
 Kama inavyo onekana pichani Mazishi hayo yalitanguliwa na ibada iliyofanyika  nyumbani kwa Marehemu

 Adv.Dominic Daniel katika Ibada ya Mazishi ya Marehemu Bi Theresia Kokwikiriza Laurent
Sehemu ya waombolezaji wakiendelea na Ibada ya Mazishi.


 Waumini wa kiendelea na Ibada.
Ibada ya misa ya kumwombea marehemu kabla ya kuelekea eneo la makaburi
 Mwl. Kagirwa akitoa neno kama msemaji Mkuu wa familia.
Neno kutoka kwa Mwl. Leonidas Kagirwa msemaji wa familia.
Jeneza lenye mwili wa Bi Theresia K.Laurent likifungwa mara baada ya zoezi la kushuhudia.
 Jeneza  lenye mwili wa Ma Theresia Kokwikiriza Laurent likiwa eneo la kaburi
Jeneza lenye mwili wa BiTheresia Kokwikiriza Laurent likiingizwa  kaburi
 Ndugu Ishengoma Bilikwija pichani katikati, mmoja wa waombolezaji.
 Ndugu Justuce Lugahibula na Mzee Mpinzile,marafiki wakubwa wafamilia wameweza kushiriki kikamilifu shughuli ya Mazishi hayo.
 Watu kutoka maeneo mbalimbali wameweza kuhudhuria na kushiriki Mazishi hayo
Padre akiweka udongo kaburini kama Ishara ya kumuaga marehemu Ma Theresia.
'Sisi ni mavumbi na mavumbini tutarudi' Padre akiweka udongo Kaburini.


 Baada ya Mapadre kuweka Udongo zoezi likaendelea kwa Ndugu wa familia ,watoto na Wajukuu wa Marehemu  Ma Theresia Kokwikiliza Laurent 
Utaratibu wa kuweka udongo ukiendelea.


 Bi Theresia Kokwikiriza apumzishwa kwenye nyumba yake ya milele jumatatu Aug 25,2014.
Zoezi la kuweka udongo likiendelea...
Umati  wa waombolezaji ukiwa makaburiki ukishiriki katika mazishi hayo.
Padre anatoa utaratibu kuhusu mashada ya maua na mishumaa

 Utaratibu wa kuweka mashada ya mauwa kwa pamoja
Wakiweka mashada ya maua na kuwasha mishumaa ...
Ndugu Justuce akiweka Mshumaa kaburini baada ya kuweka shada la maua 
Mzee Mpinzile na Justuce mara baada ya kuweka Mishumaa kaburini
Wakikamilisha zoezi la kuwasha mishumaa ...

Wajukuu wa marehemu Katika moja ya  picha ya kumbukumbu .
Wadau wakiwafariji wafiwa mara baada ya shughuli ya maziko.
Baadhi ya waombolezaji wakiwa ndani
Mc Mwongozaji wa shughuli ya maziko hayo akitoa utaratibu
Dominic na Nelson wajukuu wa marehemu wakiteta jambo.
Mdau Haruna Goronga akitowa pole kwa mfiwa.
Ndivyo inavyo onekana Nyumba yake ya Milele Bi Theresia K. Laurent
Haya ndiyo yalijili katika shughuli ya Mazishi ya 'Omwamikazi' Bi Theresia aliye  jaliwa uzao wa watoto 11 katika ndoa yake, wavulana walikuwa 7(saba) na wasichana wanne(4)  
Lakini kwa mapenzi ya mwenyezi Mungu waliobahatika kukua ni watoto 8,ikiwa ni wavulana watano na wasichana watatu, hadi anaaga dunia ameacha watoto sita (6),wavulana watatu na wasichana watatu wengine walitangulia mbele ya haki. 
Marehemu Bi Theresia ameacha wajukuu 30 na vitukuu 16
Baadhi ya wadau waliohudhuria mazishi hayo wakipata huduma ya chakula
Baba Nelson na familia yake wakitoa pole kwa Mwl.Kagirwa, ambaye ni mtoto wa Marehemu 
 
Mzee Majid Mzuzu na Mwl. Joseph Katalahiya ni sehemu ya waombolezaji 
Ndugu Thomas naye ameweza kushiriki mazishi haya 
BUKOBAWADAU BLOG TUNATOA  POLE KWA WAFIWA WOTE!!

Next Post Previous Post
Bukobawadau