Bukobawadau

VURUGU ZAZUKA MJI WA BALTMORE MAREKANI

Vurugu kubwa za mapigano baina ya polisi na waandamanaji zimetokea nchini Marekani katika mji wa Boltimore, baada ya maziko ya kijana Freddie Gray ambaye alikufa kutokana kujeruhiwa alipokuwa mikononi mwa polisi mapema mwezi huu.
Hali ya hatari na kutotembea hovyo imetangazwa katika mji huo kufuatia vurugu hizo.
Kifo cha Freddie Gray ambaye ni kijana mweusi mmarekani mwenya asili ya kiafrika kimesababisha maswali mengi kuhusu matumizi ya nguvu za ziada ya polisi dhidi ya raia wa marekani wenye asili ya kiafrika.

Hata hiyo Msemaji wa polisi wa Baltimore Captain Eric Kowalczyk amesema vurugu hizo pia zimesababisha maafisa wake kujeruhiwa na wengine wapo katika hali mbaya.
Next Post Previous Post
Bukobawadau