
Kufanikiwa ni ndoto ya kila mmoja wetu, hatua ya kwanza ya mafanikio ni kuwa na mawazo chanya, Kwa sasa Kijana Ashraphanajishughulisha kama Meneja Masoko wa Kampuni iitwayo TRAVELPORT (T) LTD iliyopo jijini Dar es Salaam ,Akiongea na Bukobawadau Media amesema;''Kwa muda mrefu nimetamani kuwa mwanasiasa nikiwa na lengo la kuwawakilisha wananchi wenzangu katika fursa mbalimbali ''
Akimnukuu mwanafalsafa mahiri aitwae PLATO ,Kijana Ashraph anasema 'wale wenye weledi, mahiri na waadilifu wasiopenda siasa hujikuta wakitawaliwa na watu wa hovyo. Hivyo yeye ni mmoja kati ya walio weledi na waadilifu'
Tunawatakia usiku mwema!
4 comment:
Safi sana kijana. Ulipokosea ni hapo kwenye kijani.
Nanjua sana Huyu kijana,,,Anao Weledi wa Hali ya juu sana na ni mtu makini katika utendaji kazi.Anapenda Umoja na mshikamano..ipo siku atakuwa na nafasi nzuri katika taifa hili...Lakini namsihi ili atimize malengo yake hayo hana budi kuzisoma vizuri alama za nyakati hizi tulizonazo kwa sasa.
Ushauri umepokelewa na ngoja tuufikiri kwa kina
Nadhani nchi hii tufike kipindi cha kuchagua watendaji wenye kumaanisha wanachokizungumza kuliko vyama.
Post a Comment