MKUU MPYA WA WILAYA YA NGARA MKOANI KAGERA AAPISHWA RASMI NA MKUU WA MKOA WA KAGERA

Mkuu mpya wa Wilaya ya Ngara mkoani Kagera Bi Honoratha Chitanda aliapishwa rasmia na Mkuu wa Mkoa wa Mkoa wa Kagera Mhe. Johna Mongella kushika wadhifa huo wa kuiongoza Wilaya ya Ngara na kukabidhiwa rasmi nyaraka mbalimbali za kumsaidia kutekeleza majukumu yake ipasavyo.
Bi Honoratha Chitanda Mkuu mpya wa Wilaya ya Ngara aliapishwa Agosti 12, 2015 katika hafla fupi iliyofanyka katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Kagera na kuhudhuriwa na viongongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wananchi.


Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. John
Mongella alimpongeza Mkuu wa Wilaya ya Ngara Bi Chitanda kwa kuteuliwa na
kusistiza kuwa jukumu la kuteua wasaidizi wake ni la Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
yeye mwenyewe na anapoona inafaa kufanya hivyo.
Bi Honoratha Chitanda kabla ya
kuteuliwa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Ngara alikuwa
mstaafu katika wadhifa wa Umakamu
wa Rais wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) tangu Mei 2015. Na kabla ya
kuteuliwa kwake Wilaya ya Ngara ilikuwa inaongozwa na Bw. Costantine Kanyasu
aliyeachia wadhifa huo kwa kugombea ubunge Jimbo la Geita Mjini.
Katika picha ya pamoja