Bukobawadau

Mkurugenzi wa World Share Kim, Na Ra atoa taa za sola 70 ili kuwasaidia waathirika wa Tetemeko kagera.

WAATHIRIKA wa tetemeko la Ardhi wanaoishi katika maeneo ya Bilongo kata Minziro kijiji kigazi wameilalamikia serikali kutokana na msaada mdogo unaotolewa kwao kutokidhi mahitaji yao kulingana na walivyothirika.

Malalamiko hayo yametolewa kutokana  kupatiwa vyakula kidogo na wakati mahitaji yao yakiwa ni mkubwa kwakuwa athari waliyoipata imewapelekea kuharibu kila kitu chao na kusababisha kukosa chakula hadi sasa.
Hayo yalibainishwa na baadhi ya wananchi waliopoteza makazi yao wakati wa tetemeko ambao Yasinta Patrick na Agnes Sedhalio walibainisha hayo wakati walipotemberewa na mkurugenzi wa (World Share) Shirika linalojishughusha na watoto yatima na alibino  Kim,Na Ra raia wa kolea kusini ambae pia alitoa taa za sola 70 kwaajili ya waathika hao ili ziweze kuwasaidia nyakati za usiku wanapokuwa katika mahema yao ambayo ni makazi yao muda.
Hata hivyo Yasinta Patrick mama mwenye watoto saba alisema kuwa serikali ilipo pereka misaada ili waperekea mchere kilomoja na nusu, unga kilomoja na Nusu  Maharagwe kilo mbili, na Sukari nusukilo, pamoja na bisukuti pakiti tano.
Patrick alisema kuwa chakula hicho wanacho pewa na serikali hakitoshi katika familia ya watoto saba maana kwa sasa hawana makazi zaidi wanautumia muda mwingi kulinda mali zao.

"Jamani Serikali itufikilie maana chakula hicho tunachopewa hakitoshi hata siku mbili kwa familia kama yangu mimi mwenye watoto wengi na mimi pia"alisema Patrick

Agnes Sedhalio alisema kuwa serikali iwatumie watu wanaoaminika katika kugawa misaada hiyo kwa jamii maana wanapo kuja kutugawia hiyo misaada hata hawatuthamini kama sisi ni watu kama watu wengine.
"Hivi unga kilomoja na nusu na mchere kilomoja na nusu kweli unatosha au nikutudhihaki' mfano mimi wananiletea bistukut ili niwape watoto wale kweli au maji chupa moja ni kwanini wasitulete chakula moja kwa moja tukajua moja kwakweli inasikitisha sana kwa mambo tunayofanyiwa"alisema Sedhalio
Naye mwenyekiti mstafu Godfry Kagoro alisema kuwa katika kijiji cha Kampaini kilichopo mpakani mwa Tanzania na Uganda alisema kuwa katika eneo hilo kuna zaidi ya wananchi 200 lakini waliopewa mahema na hivyo vyakula kidogo ni familia saba tu wanaoishi barabarani tu. 

Kagoro alisema kuwa tetemeko hilo baada ya kupita limeharibu utalatibu wa maisha ya kawaida hivyo kuna hatali ya watu kufa na njaa.

"  Kwa sasa hatuna chochote kile zaidi ya kuanza ujenzi wa nyumba kwa upya na hatujui hatima ya serikali kwa familia zetu waliokuwa wanakweda kuhangaika kutafuta riziki sasa hawaendi, wakati mwingine tunaogoka kwamba tukitoka litajirudia tena jamani  serikali itupe msimamo kamili juu ya tetemeko hili"alisema Kagoro
Pia wananchi hao wametoa ombi lao kwa mbunge wa jimbo la Nkenge Dr Diodorus Kamala kuludi jimboni ili aweze kuwasaidia katika kuwabaini waathilika kiundani maana walio wengi hawaja fikiwa na watoa tathimini.
Mwisho.

Next Post Previous Post
Bukobawadau