Bukobawadau

SHUKRANI TOKA KWA FAMILIA YA AL HAJJI ABBAKARI GALIATANO KUFUATIA MSIBA WA MZEE WAO !

 Viongozi wa Dini wakiwaongoza Maelfu ya wananchi kushiriki Dua maalum ya kumuombea Alhaji Abbakari Rajabu Galiatano kabla ya shughuli ya  mazishi yaliyofanyika nyumbani kwake  kijijini Buganguzi Muleba siku ya Jumapili Julai 9,2017.
Shukrani:Familia ya Al hajji Mzee Abubakari Rajabu Galiatano inapenda kutoa shukrani nyingi sana na za kipekee kwa ndugu,Jamaa ,marafiki,majirani na viongozi wa Dini na siasa wote kwa kujitoa kwa hali na mali kufanikisha shughuli za mazishi ya Mzee Abubakari Rajabu Galiatano aliyefariki siku ya Jumamosi tarehe 8 Julai,2017 na kuzikwa siku ya Jumapili Julai 9,2017 nyumbani kwake kijijini Buganguzi Muleba.
Ni vigumu kushukuru mtu mmoja mmoja kutokana na wingi wenu na kwa jinsi kila mmoja alivyojitoa na kuonesha upendo wa dhati kabla na baada ya mazishi. Tunaweza kujaza kurasa 200 kama hizi na tusiwe tumehitimisha robo tu ya shukrani zetu kwa kila mmoja wenu.
TUNAWAOMBEA KWA MOLA AWAJALIE KATIKA KILA JAMBO. 
Pamoja na hayo shukrani za kipekee ziwaendee uongozi na madaktari wa hospitali zifuatazo :Hospital Aga Khan,Hospitali ya St.John Bukoba,hospitali ya Mkoa Kagera, Rabinisia Dar es Salaam,CCBRT na Hospitali ya Taifa Muhimbili.
Asanteni! Asanteni! Asanteni! na Mungu awabariki katika maisha yenu.
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un..!!
 Shekh wa Mkoa wa Kagera Sheikh Haruna Kichwabuta akitoa nasaha zake katika msiba huo mkubwa kwa wanakagera
 Ndugu Al Amin Abdul na Bwana Sued Kagasheki wakielekea eneo la makaburi kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Mzee Abubakari Rajabu Galiatano
 Mamia ya waombolezaji wakiongozana kuelekea eneo la makaburi
 Waombolezaji wakielekea eneo la makaburi kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Mzee Abubakari Rajabu Galiatano
 Endelea kuwa nasi kwa matukio zaidi ya picha....
Next Post Previous Post
Bukobawadau