Bukobawadau

DUA NA SHUKRANI MWAKA MMOJA KIFO CHA MZEE KASSIMU KARUANDILA - KITENDAGURO BK

 Familia ya Marehemu mzee Kassimu Karuandila wa Kitendaguro Bukoba pamoja na familia ya Bi Farida Kassimu na Mama yao Christer Karuandila inapenda kuwashkuru ndugu jamaa na marafiki wote kwa upendo na faraja mlivyowapatia katika kipindi chote cha msiba mpaka kufikia kipindi cha Matanga (Dua ya Mwaka mmoja) ya Mzazi wao Marehemu Mzee Kassimu Karuandila Shughuli ya Dua ilifanyika siku ya Jumamosi Aug 12,2017 Nyumbani kwake Kitendaguro Bukoba.
Wakati wa Uhai wake Marehemu Mzee Kassimu aliwahi kuwa Meya wa Mji wa Bukoba.
 Baadhi ya watoto wa familia ya Marehemu Mzee Kassimu Karuandila,wa mwisho kulia ni Bi Farida Karuandila ambaye ndiye mtoto mkubwa katika familia hiyo.
Mzee  Abdul Katabaro katika picha ya pamoja na Mama Christer Karuandila mama wa familia.
 Matukio ya awali hii ni picha ya pamoja ya marafiki na wanachama  maarufu kama (Sauti ya wamama)kutoka kushoto ni Bi Leonida,Bi Beatrice, Da' Mercy ,Da' Farida Kassimu na Bi Jeanifer Murungi kichwabuta
 Bwana Abdallah Idrisa akiwa na binti wake Sajidah
 Watoto wa Marehemu mzee Kassimu pichani ni Mrs Towo na Teddy Kassimu
 Katikati ni Vijana wa kiume wa kuzaliwa na Marehemu mzee Kassimu Karuandila,Bw Abdul na Lihad wakiwa na majirani zao muda mchache kabla ya Shughuli ya dua kuanza
 Bi Anna Luangisa, Ms Jamila na Mrs Daudi Kibogoyo wakicheck na Camera yetu mapema kabla ya shughuli ya dua ya kumuombea Mzee Kassimu Karuandila ikiwa ni mwaka mmoja tangu kifo chake
Nikuombe wewe msomaji wetu tuwe wote mpaka mwisho kwa mtiririko mzima wa matukio ya picha yaliyojiri katika Shughuli Dua iliyoongozwa na Sheikh Kakwekwe ,sheikh wa Wilaya ya Bukoba Mjini Aug 2017.
 Mzee Selemani Kabyemela akishiriki dua ya kumuombea rafiki yake Marehemu Mzee Kassimu
 Bwana Abdul na Mzee Abdul Katabaro wakiendelea kushiriki Dua hiyo
 Sehemu ya waalikwa waliohudhuria shughuli ya Dua ya kumuombea mzee Kassimu Karuandila.
 Ndugu Lihad Kassimu akimlaki rafiki yake Optaty Henry wakati anawasili kushiriki dua ya kumaliza matanga (Mwaka mmoja) kifo cha Mzee Kassimu Karuandila
 Wadau kwa pamoja wakiwasili eneo la tukio kijijini Kitendaguro Bukoba
 Mr. Charles Luangisa pichani kushoto.
 Sheikh Kakweke akitoa nasaha zake
 Neno kutoka kwa Sheikh Mussa ,Sheikh wa mtaa wa Kitendaguro Manispaa Bukoba
Mzee Hamisi Mnyonge pichani kushoto
Sehemu ya Waumini wa dini ya Kiislamu wakiomba dua ikiwa Mwaka mmoja tangu kifo cha Mzee Kassimu Karuandila.
 Bro Majid Kichwabuta wakati wa utambulisho.
Bi Chiku mama Nabir akishiriki shughuli ya Dua hiyo
Taswira mbalimbali Wakati Kisoma kinaendelea
 Sehemu ya wanafamilia wakati Dua ikiwa inaendelea..
Al hajji Sadick Galiatano wa pili kutoka kulia akifurahia jambo.
 Bi Jeanifer Murungi kichwabuta na Bi Mercy wakiendelea kushiriki kisomo cha Dua .
 Jumanne Bingwa na Bwana Katibu Optaty Henry
 Baadhi ya wadau walioshiriki shughuli ya Dua ya Mwaka mmoja tangu kifo cha Mzee Kassimu Karuandila iliyofanyika nyumbani kwake Kijijini Kitendaguro Bukoba.
 Ndugu na jamaa waliweza kujitokeza kushiriki kisomo cha Dua ya mwaka mmoja kifo cha Mzee wetu, Mzee Kassimu Karuandila
Mr. Rugomola akiwa ameungana na familia ya marehemu Mzee Kassimu Karuandira katika shughuli ya Dua ya kumuombea mzee wao.
Mara baada ya Dua kinachofuata ni watu wote kupata Ubani ulioandaliwa katika shughuli hiyo
Katika kuwajibika anaonekana  Bi Jeanifer Murungi kichwabuta
 Utayari kuelekea kupata huduma ya Chakula
 Ma Rachel Barongo akipata huduma ya Chakula.
Watoto wakipata huduma safi ya Chakula
Hakika shughuli ilikuwa vyema kama wanavyo onekana watoto wakifurahia msosi



Sehemu ya wanaume wakati huduma ya Chakula inaendelea
Sehemu ya wanawake wakiendelea kupata msosi
 Ndugu Jumanne Bingwa akiteta jambo na Bi Farida Kassimu
Mrs Towo,Beatrice na Bi Farida Kassimu katika picha ya pamoja
 Sehemu ya marafiki na wanafamilia katika picha ya pamoja.
Muendelelezo wa picha za kumbukumbu kwa ndugu na marafiki wa familia
Kutoka kushoto Bi Sharifa Karwani,Kadigi ( Mrd Daudi Kibogoyo) na Mrs Towo
Bi Farida, Mercy na Mrs Balyagati
Bwana Charles Luangisa akisalimiana na Mzee John Lujwangana
Jack Kibogoyo,Abdul Kassimu na Nina Pocoloco katika picha maalum ya kumbukumbu kupitia Bukobawadau
 Mzee Abdul Katabaro akibadilishana mawazo na Jumanne Bingwa pamoja na Majid Kichwabuta.
Ms Jamila akiwa na Simu yake ya kiganjani
 Bi Farida Kassimu Karuandila pichani akiwa tayari kushiriki Dua ya kumuombea mzazi wake
 Bi Anna Luangisa pichani katika pozi moja matata
Wakati Bi Beatrice akipata msosi mara baada ya shughuli nzima kukamilika
Wakuitwa Kadigi au Mrs Daudi Kibogoyo wakati akipata msosi
Mapema kabisa Camera yetu ikiangaza maeneo ya Jikoni


Kitu cha biriani Masala kilihusika pia...
Muonekano wa eneo la tukio sehemu ya wanawake kabla ya shughuli kuanza.

Muonekano wa kaburi la Marehemu Mzee Kassimu Karuandila,tumuombee  kwa Mungu azidi kumpa pumziko.
Inna lillahi wa inna ilayhi raji'un!
Sasa unaweza kupata habari mpya za uhakika kilahisi zaidi kwa kudownload Application ya Bukobawadau kwenye simu yako kutoka Play Store >>  BUKOBAWADAU APP
Next Post Previous Post
Bukobawadau