Bukobawadau

KANISA LATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU BIHARAMULO

Kanisa la FPTC  linalotoa huduma za kiroho  katika wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera kwa kushirikiana na wafadhili kutoka nchini  Finland limetoa msaaa wa baiskeli 24 na kilo 200 za mahindi  kwa watoto 30 wenye ulemavu wa viungo na  mtindio wa ubongo kwa gharama ya  Sh10.88 milioni
Akikabidhi  msaada huo jana  Mratibu wa mradi wa kuhudumia walemavu katika kanisa hilo  Lizia Masele alisema watoto hao wenye mahitaji maalum wapata Baiskeli 10 za kawaida , Wheelchair 10, Trycycle nne na blocks seti mbili kwa ajili ya wanafunzi    wa shule ya msingi Kabindi na Biharamulo mjini.
Masele alisema kanisa hilo kwa kushirikiana na wafadhili wa Finland wanafanya kazi ya kutoe elimu kwa jamii kuhimiza haki za watoto, kusaidia watoto wenye ulemavu kupata elimu, kuwanunulia vifaa watoto wenye mahitaji maalum na kuwatibisha walemavu wenye kuwa na maradhi yanayotibika.  
“Shughuli zetu tunashirikiana na mfadhili Maria Holmberg kutoka Finland ambaye ni mshauri wetu lakini tukishauriana na watendaji mbalimbali katika ofisi ya mkurugenzi  wa wilaya hii na kupata ufanisi mkubwa” Alisema Masele
 Pichani kushoto Diwani wa Kata Nyamahanga Amon Movati na Afisa tarafa ya Nyarubungo wilayani Biharamulo mkoani Kagera Nyambuli Siangi (pichani kulia) wakitoa msaada kwa watoto wenye ulemavu
 Afisa ustawi wa Jamii Ladislaus Raulent na Afisa tarafa ya Nyarubungo Nyambuli Siangi, waliomba wafadhili hao kuendelea kusaidia  watu wenye ulemavu wakati serikali ikitafuta fedha za kuboresha mazingira yanayowazunguka, hasa katika shule zenye wanafunzi wenye ulemavu na sehemu za kazi kwa watu wazima.
Pia Afisa ustawi wa jamii aliwashauri baadhi ya wazazi au walezi kutumia rasilimali zinazowazunguka kuwapatia chakula chenye lishe watoto wao hata kama wanakabiliwa  na ulemavu   waweze kukua kiafya badala ya kupatwa na utapiamlo unaodhoofisha afya zao.
 Hata hivyo mfadhili wa kanisa hilo na watoto wenye mahitaji maalum kutoka Finland Maria Holmberg alisema nchi yake imepunguza utoaji misaada kwa kanisa hilo kwa sababu ya  changamoto za kiuchumi duniani  ambapo kanisa haliwafikii walengwa kwa kukosa usafiri wa kuwafikia kutokana na ubovu wa barabara vijijini
 Maria Holmberg kutoka nchini Finland (mzungu) akiwakabidhi baiskeli za aina mbalimbali  watoto  wenye ulemavu wakiwa na wazazi wao katika kanisa la FPTC lililopo kata ya Nyamahanga wilayani Biharamulo mkoani Kagera
Maria Holmberg kutoka nchini Finland akiwakabidhi baiskeli za aina mbalimbali  watoto  wenye ulemavu wakiwa na wazazi wao katika kanisa la FPTC lililopo kata ya Nyamahanga wilayani Biharamulo mkoani Kagera  

Picha  na Shaaban Ndyamukama
Next Post Previous Post
Bukobawadau