Mkuu wa Mkoa Meja Jenerali Mstaafu Salum M. Kijuu afanya ziara ya
kukagua huduma za afya Mkoani Kagera na kuzindua unyunyiziaji wa dawa ya
kuua viluilui katika mazalia ya mbu ili kupunguza tatizo la malaria
mkoani hapa.
Ziara hiyo iliyoanza tarehe 12 Septemba, 2017 katika
Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba Mhe. Kijuu alizindua ugawaji wa
vitambulisho vya kupata huduma ya afya kwa wazee ili watibiwe katika
vituo vya afya bure bila malipo yoyote.
Katika ziara hiyo Mkuu wa
Mkoa alilenga kukagua na kujihakikishia uwepo wa dawa katika vituo
mbalimbali vya afya kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi. Pili
alilenga kuhamasisha wananchi kujikinga na kuchukua hatua za kupambana
na ugonjwa wa Malaria ili kupunguza maambukizi ya ugonjwa huo katika
Mkoa wa Kagera.
Aidha, Mkuu wa Mkoa alilenga kuhamasisha vituo
vyote vya afya kutumia mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya
kielekitroniki ili kuongeza mapato yatayoboresha huduma kwa wananchi.
Katika ziara hiyo Mhe. Kijuu alijihakikishia kuwa dawa zipo za kutosha
kwenye vituo na kutoa rai kwa wananchi kufika katika vituo hivyo pindi
wanapohisi wanaumwa ili kupatiwa huduma za matibabu.
Katika ziara
hiyo Mhe. Kijuu aliwasistiza watendaji wa Halmashaui za Wilaya
kuhakikisha wazee wanapatiwa vitambulisho na kusema kuwa wazee hao
wakati wa ujana wao walizalisha na kulitumikia taifa kwa nguvu zao zote
na sasa ni wakati wao kuhudumiwa hasa kupatiwa huduma za afya bure bila
kutozwa fedha zozote.
Aidha, Mhe. Kijuu alimpongeza Rais John
Pombe Magufuli ambaye naiongoza Serikali ya Awamu ya Tano kwa
kuwakumbuka wazee na kuwapatia vitambulisho ambavyo vitawaruhusu wazee
wa Tanzania kupatiwa huduma za afya bure bila malipo.
Katika
Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba tayari wazee 900 wametambuliwa na
kupewa vitambulisho, Halmashauri ya Wilaya ya Missenyi tayari wazee 1500
wametambuliwa na wanatarajiwa kupatiwa vitambulisho na Halmashauri ya
Wilaya ya Bukoba Zaidi ya Wazee 200 tayari wamepatiwa vitambulisho vya
kupatiwa huduma ya afya bure.
Agizo ni kuwa Halmashauri zote
zinatakiwa kuwatambua wazee na kuwapatia vitambulisho hivyo. Aidha Mhe.
Kijuu aliziagiza Halmashauri zote kuhakikisha zinanyunyizia dawa ya kuua
viluilui katika madimbwi, kandokando ya mito ili kuharibu mazalia ya
mbu, pia kuhakikisha Halmashauri zote zenye shehena ya dawa katika
maghara ya dawa, dawa hizo zisambazwe vituoni ili kutoa huduma kwa
wananchi.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Kagera Dk. Thomas Rutachunzibwa
katika ziara hizo alitoa rai kwa watendaji wa Halmashauri kuona umuhimu
wa kufunga mfumo wa ukusanyaji mapato kwa njia ya kielekitroniki ili
kuongeza mapato katika vituo hivyo jambo ambalo litaboresha utoaji wa
huduma za afya kwa wananchi na kuacha utegemezi na vituo kujiendesha
vyenyewe kwa makusanyo yao wenyewe.
Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu
alitembelea vituo vya afya Rubale Wilayani Bukoba, Buyango na Bunazi
Wilayani Missenyi, pia na Kituo cha Afya Zamzam Manispaa ya Bukoba.
Vilevile alitembelea maeneo dawa ya kuua viluilui inakonyunyiziwa hasa
katika madimbwi na maji yaliyotuhama
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comment:
Post a Comment