Bukobawadau

RAIS DKT. MAGUFULI NA MWENYEJI WAKE RAIS WA UGANDA YOWERI MUSEVENI WAWEKA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA BOMBA LA MAFUTA GHAFI LA KUTOKA HOIMA NCHINI UGANDA HADI TANGA KATIKA WILAYA YA KYOTERA MUTUKULA NCHINI UGANDA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akishikana mkono na kupongezana na Mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa Bomba la Mafuta ghafi litakalo toka Hoima nchini Uganda hadi eneo la Chongoleani mkoani Tanga. Sherehe za uwekaji wa jiwe hilo zimefanyika katika eneo la Mutukula Wilayani Kyotera nchini Uganda

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wakisikiliza maelezo ya namna ya bomba hilo la mafuta ghafi litakavyojengwa na kuanza kufanyakazi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta wakijadiliana jambo mara baada ya kupewa maelezo ya mradi huo mkubwa wa bomba la mafuta ghafi.

Jiwe hilo la Ufunguzi la Ujenzi wa Bomba hilo la Mafuta ghafi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli na Mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni wakiondoka katika eneo la Mutukula mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la bomba la mafuta.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasili pamoja na Mke wa Rais wa Uganda Mama Janeth Museveni katika eneo la mpaka wa Tanzania Mutukula kabla ya ufunguzi wa Kituo cha pamoja cha huduma za mpakani kwa upande wa Tanzania na Uganda
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Rais wa Uganda Yoweri Kaguta Museveni mara baada ya kuwasili upande wa Tanzania kabla ya ufunguzi wa Kituo cha pamoja cha huduma za mpakani kwa upande wa Tanzania na Uganda.
Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli akiwasili pamoja na Mke wa Rais wa Uganda Mama Janeth Museveni wakiangalia ngoma katika eneo la Mutukula upande wa Uganda.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mke wake Mama Janeth Magufuli wakifurahia ngoma za asili za  watoto wa Uganda mara baada ya kuwasili nchini humo huku Rais wa Uganda Yoweri Musevini akitazama watoto hao.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mwenyeji wake Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakati wa nyimbo za mataifa ya Tanzania na Uganda zikipigwa katika eneo la Uganda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakifungua Ofisi za Kituo cha pamoja cha huduma za mpakani kwa upande wa Tanzania. Wanne kutoka kushoto ni Mke wa  wa Rais Mama Janeth Magufuli akishuhudia pamoja na Mke wa Rais Museveni Mama Janeth Museveni wa kwanza kushoto.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na Rais wa Uganda Yoweri Museveni wakizungumza na mamia ya wananchi hawaonekani pichani katika eneo la Kyatera nchini Uganda mara baada ya ufunguzi wa Bomba la Mafuta. PICHA NA IKULU
Next Post Previous Post
Bukobawadau