Balozi Diodorus Buberwa Kamala amezitaja sheria zilizofanyiwa marekebisho ni Sheria ya Madini, ya Ushuru wa Bidhaa, Kodi ya Mapato, Mamlaka ya Serikali za Mitaa ya utozaji kodi ya majengo,na ya VAT.Amesema;Marekebisho hayo pia yanakusudia kuanzisha vituo vya ununuzi wa madini katika maeneo ambako masoko ya madini hayakuwepo, na kuweka utaratibu wa uingizaji madini nchini.
Pia katika Mkutano huo Mbunge Balozi Dr.Kamala ameongelea maandalizi ya Mkutano Mkubwa ujulikanao kama 'Missenyi Investment Forum' unaoandaliwa na Ofisi yake kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya pamoja na Halmashauri,Lengo kuu la mkutano huo ni kukuza na kubahinisha fursa za biashara katika sekta mbalimbali Wilayani Missenyi.
Ndugu Kutone mdau wa maendeleo Missenyi akitoa hoja yake kwa Mbunge wa Jimbo la Nkenge
Bwana Shahidu Chagulani pichani
Mh.Twaha Diwani wa Kata Kasambya na Mh. Lidia Diwani viti maalum wakimsikiliza kwa makini katibu wa Mbunge wa Jimbo la Nkenge Ndugu Peter Mwafiwa.
Katibu wa Mbunge wa Jimbo la Nkenge kwa tarafa ya Missenyi Ndugu Peter Mwafiwa 'Shegede' pichani akitolea jambo ufafanuzi katika mkutano huo uliofanyika Viwanja vya shule ya Msingi Kasambya.
Baadhi ya wananchi wakifuatilia kinachojiri
Muendelezo wa matukio ya picha
0 comment:
Post a Comment