Bukobawadau

Asecdo wafanya nomaaaaaaaaaaa!!!!!!!!Wachoma nyumba moto na kuaribu Mali..

Kundi la vijana waendesha Pikipiki mjini Bukoba maarufu kama Asecdo wamefanya uwamuzi wa kujichukulia sheria mkononi kwa kuchoma Nyumba moja moto na matuka mawili mali za Bwana John Kaitaba mkazi na mzaliwa wa maeneo ya Kibeta kilometa nne nje kidogo ya mji wa Bukoba.

Tukio hilo limetokea leo majira ya saa 5 asubuhi.Wakiongea na bukobawadau majirani wa Ndg John wamedai:Vijana hao maarufu kama Asecdo wamefikia uwamzi huo kwa sababu wanamtuhumu Ndg John kama jambazi,mualifu wa kuteka na kufanya mauwaji asa ya waendesha pikipiki na kuhifadhi waalifu kwenye Nyumba yake.
Familia hii ilikuwa ikipanga kwenye nyumba iliyo chomwa moto japo walipewa tarifa mapema ili watowe mali zao ila inatia uchungu,huruma na simanzi kubwa saana kama unavyo waona watoto wadogo hawana hili wala lile!!
Baadhi ya wadau wakishuhudia namna Nyumba inavyozidi kuteketea kwa moto.
Kikosi cha zima moto cha Manispaa ya Bukoba kikijaribu kuzima mote wakati nyumba imeisha teketea.
Next Post Previous Post
Bukobawadau