Bukobawadau

NYUMBA YA MDAU MZEE ANTHONY YAUNGUA MOTO USIKU HUU!!!!!ni maeneo ya Kashai Center

Moto ukiendelea kuunguza Nyumba ya Mzee Anthony wa Kashai Bukoba muda huu.
 Mripuko mkubwa wa moto kabla kikosi cha zima moto hakijafika...!!!!
 Moto ukizidi kushika kasi
Mzee maarufu jirani na ajali hii ya moto ni Sheikh Idrisa (mwenye kibaragashia) anaonekana akitoa ushirikiano kwa kuokoa mali zilizosalimika.
 Kikosi Cha zima moto cha Manispaa ya Mji Bukoba kikiendelea na kazi ya kuzima moto unao endelea kuteketeza Nyumba ya Mzee Anthony iliyopo Kashai.
 Wadau wakiendelea kushuhudia
 Nimeshuhudia  Jeshi la polisi kwa kushirikiana na Kikosi cha zima moto wakifanya kazi kwa jitiada kubwa sana pichani ni Mdau Peter Matagi.
Shughuli ya kuzima moto inaendelea.
 Mashuhuda wa  tukio hili wameuelezea mtandao wa bukobawadau kuwa Chanzo cha moto huu ni Mshumaa uliokuwa unawaka katika mojawapo ya Chumba katika nyumba hii.
Mmoja kati ya wapangaji wa nyumba hii akiwa katika masikitiko makubwa.
Sehemu ya mashuhuda katika  tukio hili lililotokea usiku huu  majira ya saa 2.30
Bukobawadau Blog tunatoa pole kwa wadau waliofikwa na TUKIO hili.
 Mc baraka (blogger) akiwajibika .
Ni Full taflani ukizingatia na idadi kubwa ya wadau wanaoishi katika eneo hili la kashai, tukio limetokea majira ya saa 2.30 usiku ni njia panda ya kutoka kashai kuelekea eneo la Matopeni.
 Baadhi ya Mali zilizosalimika.
 Mali nyingi zimetekea kwa Moto na hizi ndizo zilizosalimika.
 Chanzo cha moto huu ni mshumaa uliokuwa umewashwa na mmoja wa wapangaji  na baadae kushika kwenye godoro  na kusambaa.

BUKOBAWADAU BLOG TUNATOA POLE KWA WOTE WALIOFIKWA NA JANGA HILI !!!!
Next Post Previous Post
Bukobawadau